Tuesday, 16 June 2015

list ya wanamichezo wanaolipwa mkwanja mrefu duniani hii hapa maywether akiongoza


Floyd Mayweather Jr, mwanamichezo anayelipwa zaidi ulimwenguni
Bondia Floyd Mayweather Jr ndio mwanamichezo aliyeingiza pesa nyingi zaidi dunia katika kipindi cha miezi 12 iliyopita kwa mujibu wa jarida la Forbes.
Mayweather ameingiza kiasi cha dola milioni 300 katika kipindi cha miezi hiyo na fedha nyingi ikiwa imepatikana kutoka na pambano lake na bondia Manny Pacquiao.
Manny ameshika nafasi ya pili katika orodha hiyo huku nyota wa kandanda Cristiano Ronaldo akiwa katika nafasi ya tatu kwa wanamichezo waliotengeneza pesa nyingi.
Orodha kamili ipitie katika tovuti ya bbcswahili.com
Ifuatayo ni orodha kamili ya wanamichezo hao
1. Floyd Mayweather, US, US$300m (£194m).
2. Manny Pacquiao, Philippines, $160m (£103.4m)
3. Cristiano Ronaldo, Portugal, $79.6m (£51.4m)
4. Lionel Messi, Argentina, $73.8m (£47.7m)
5. Roger Federer, Switzerland, $67m (£43.3m)
6. LeBron James, US, $64.8m (£41.9m)
7. Kevin Durant, US, $54.1m (£35m)
8. Phil Mickelson, US$50.8m (£32.8m)
9. Tiger Woods, US, $50.6m (£32.7m)
10. Kobe Bryant, US, = $49.5m (£32m)

wakati mataifa ya afrika yanafanya vizuri katka soka eti tanzania tunaweza huu


Mcheza golf akiwajibika.
Michuano ya gofu ya Afrika (African golf Jacket) itakafanyika Windhoek, Namibia huku nchi kadhaa za Afrika ikiwemo Tanzania na Kenya zikitarajiwa kushiriki.
Nchi nyingine ni pamoja na Botswana, Afrika ya Kusini, Zimbabwe, Zambia, Msumbiji, Swaziland na wenyeji, Namibia, ambao watagharamia wageni wao
Makamu wa raisi wa chama cha gofu nchini Tanzania (TGU), Joseph Tango amesema mchezaji Abbas Adamu kutoka Arusha, Kaskazini mwa Tanzania atakuwa ni miongoni mwa washiriki, baada ya kushinda mara mbili michuano iliyopita na akiwa miongoni mwa wachezaji wa daraja la juu (Division A).
Wachezaji wengine wawili watachaguliwa kutoka division B na C na Tango atakuwa kiongozi wa msafara. “Tuna mategemeo wachezaji wetu watafanya vizuri na kurudi nyumbani na ushindi”, amesema Tango.

taarifa kamili ya raheem sterling kuondoka liverpool hii hapa.



Raheem Sterling

Liverpool imekataa ombi la kitita cha pauni milioni 25 na nyongeza ya pauni milioni 5 kutoka kwa Manchester City ili kumnunua Raheem Sterling.
Pia inaaminika kwamba Liverpool inamthamini mchezaji huyo wa miaka 20 kuwa na thamani ya pauni milioni 50 na kwamba haina mpango wa kumuuza .

mancity

Mchezaji huyo amehusishwa na mzozo katika uwanja wa Anfield na hivi majuzi alisema kuwa hatoweka sahihi ya mkataba mwengine katika klabu hiyo.
Hatahivyo ajenti wa Sterling Aidy Ward amedaiwa kusema kwamba hatokubali kandarasi nyengine katika klabu ya Liverpool hata akipewa kandarasi ya pauni laki tisa kwa wiki.

Kiungo wa Nigeria apigwa marufuku.


Ugo Njoku apigwa marufuku ya mechi tatu
Mchezaji wa timu ya wanawake ya Nigeria Ugo Njoku amepigwa marufuku ya mechi tatu.
Kamati ya nidhamu ya FIFA ilifanya kikao chake nchini Canada na kufikia uamuzi huo baada ya kutizama video inayomuonesha Njoku akimpiga kumbo mchezaji wa Australia Sam Kerr katika mechi ya makundi ya kombe la dunia la wanawake .
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 20 alikuwa mchezaji wa akiba na aliingia uwanjani katika dakika ya 52 ya mechi hiyo ya kombe la dunia.
Japo tukio hilo halikuonekana na muamuzi wa mechi hiyo, kamati hiyo ya nidhamu ilikaa kandokando ya kombe la dunia na kufikia uamuzi huo.
Mchezaji huyo amepigwa faini ya dola elfu tatu na mia mbili $3,200.
Mshambulizi wa Ufaransa Camille Abily aliyempiga kumbo mlinzi wa England Laura Bassett hakuadhibiwa.
The Super Falcons ya Nigeria iliambulia kichapo cha mabao 2-0 katika mechi hiyo.
Njoku sasa hataruhusiwa kushiriki mechi dhidi ya Marekani.
Haijulikani kwanini hatua sawa na hiyo haikuchukuliwa dhidi ya mshambulizi wa Ufaransa Camille Abily aliyempiga kumbo mlinzi wa England Laura Bassett.

CAF kumuunga mkono INFANTINO Urais wa FIFA

Shirikisho la soka barani Afrika CAF linamuunga mkono Infantino Rais wa shirikisho la soka barani Africa (CAF) AHMAD AHMAD amesema shir...