Friday, 22 July 2016

Huyu hapa mwanaume Anaelipwa kubikiri watoto Malawi,mtazame



Image captionEric Aniva 'Fisi ' mtajika aliyewabikiri zaidi ya watoto 104
Katika tamaduni nyingi kote duniani mwanamke anapoolewa huwa ni fahari kubwa sana akiwa ni bikira.
Mathalan ni dhihirisho la mwanamke kuwa amelelewa na kutunzwa vyema.
Ni dhihirisho la usafi.
Hata hivyo jamii moja nchini Malawi haithamini ubikira wa watoto wao wa kike.
Amini usiamini wazazi huwa wanamlipa ''Fisi'' kumbikiri binti yao punde tu anapopata hedhi yake ya kwanza.
Image captionAniva huchemsha mizizi hiyo kabla ya kuanza kubikiri watoto kwa takriban siku 3 hivi
Wanaamini kuwa binti ambaye ni bikira ni mkosi kwa jamii!
Malimwengu haya.
Wazazi na jamii kwa jumla katika maeneo mengi ya kusini mwa Malawi wamekuwa wakishikilia tamaduni hii kwa miaka na mikaka.
''Fisi'' ama wanaume wanaowabikiri watoto wa kike huchaguliwa na wazazi kuwaondolea mikosi.
Na huwa ni sherehe kubwa inayomtangulia binti kupelekwa unyagoni kisha kuwatembelea shangazi wake kabla ya kujulishwa kwa fisi.
Amini usiamini hao mafisi hulipwa takriban dola $7 kwa kila kitendo cha ngono na hao mabinti ambao wengi huwa na kati ya umri wa miaka 11-14.
Fisi mmoja katika kijiji cha Nsanje, Eric Aniva ameiambia BBC kuwa hajui kwa kweli amewabikiri wasichana wangapi, kwa sababu ni wengi.
''Kwa kweli mimi nimewabikiri zaidi ya wasichana 104," amesema. ''Hii ndiyo tamaduni yetu''.
Image captionAniva na familia yake
''Hapa mwanamke akifiwa lazima aje kwangu nimuondolee mkosi hata kabla ya kuzikwa kwa mumewe''.
''Mwanamke akiavya mimba pia kabla hajarejelea maisha yake ya kawaida ama hata kushiriki ngono na mwanamume mwengine lazima aje kwangu nimsafishe," alisema fisi huyo.
Aniva ambaye ana umri wa takriban miaka 40 ana wanawake wawili na watoto 5.
Anasema kuwa pale anaposhiriki ngono na watoto hao huwa anapewa muda wa siku 3 hivi kumsafisha na kumuondolea mkosi.
Kulingana na tamaduni zao, ikiwa mwanamke ama binti anakataa asibikiriwe huwa wanaamini kuwa jamaa zao watafuatwa na mikosi na magonjwa.

michuano ya soka barani Afrika yapata mdhamini mpya, mtazame hapa



CAFImage copyrightGETTY
Image captionKombe la Taifa Bingwa barani Afrika
Shirikisho la Soka barani Africa (CAF) limepata mdhamini mpya baada ya kumalizika kwa mkataba wake na kampuni ya mawasiliano ya Orange.
Orange imekuwa mdhamini mkuu wa mashindano makubwa ya CAF kwa miaka minane tangu 2009.
Kabla ya hapo, kampuni nyingine ya mawasiliano ya MTN ndiyo iliyokuwa mdhamini kwa miaka minne.
Sasa, mdhamini mpya atakuwa kampuni ya mafuta na gesi ya Total kutoka Ufaransa.
CAF
Image captionKombe la Mashirikisho
Kampuni hiyo itaanza kwa kudhamini michuano ya Kombe la Taifa Bingwa Afrika mwaka 2017 ambayo itaandaliwa nchini Gabon.
Thamani ya mkataba huo haijafichuliwa.

Total itakuwa mdhamini mkuu wa:

  • Kombe la Taifa Bingwa Afrika
  • Ligi ya Klabu Bingwa Afrika
  • Kombe la Taifa Bingwa Afrika kwa wachezaji wa ligi za ndani (CHAN)
  • Super Cup ya Afrika
  • Kombe la Mashirikisho
  • Kombe la Taifa Bingwa Afrika kwa Wanawake
  • Kombe la Futsal Afrika
  • Kombe la Taifa Bingwa Afrika wachezaji wa chini ya miaka 23
  • Kombe la Taifa Bingwa Afrika wachezaji wa chini ya miaka 20
  • Kombe la Taifa Bingwa Afrika wachezaji wa chini ya miaka 17

Mabishano makali kati ya BASATA na Ney wa mitego kus wimbo wake kufungiwa haya hapa














CAF kumuunga mkono INFANTINO Urais wa FIFA

Shirikisho la soka barani Afrika CAF linamuunga mkono Infantino Rais wa shirikisho la soka barani Africa (CAF) AHMAD AHMAD amesema shir...