Monday, 10 August 2015

hebu watazame hawa watoto walivyo na vipaji. all the way from maandishi matatu. U.S.A

Marekani yashambuliwa Uturuki.

 


Shambulizi nchini Uturuki
Watu wenye silaha wameufyatulia risasi ubalozi wa Marekani katika mji mkuu wa Uturuki, Istanbul.
Watu wawili walitoroka wakati maafisa wa polisi walipowafyatulia risasi lakini ripoti zinasema kuwa mshukiwa mwanamke tayari ametiwa mbaroni.
Hakuna habari zo zote za majeruhi zilizotolewa.
Shambulio hilo lilitokea muda mfupi baada ya bomu kulipuka kwenye gari moja lililokuwa limeegeshwa karibu na kituo cha polisi.
Watu kumi walijeruhiwa, wakiwemo maafisa watano wa polisi.
Inasemekana kuwa washukiwa wawili na afisa mmoja wa polisi walifariki.
Haijulikani iwapo mashambulizi hayo mawili yana uhusiano.
Uturuki imewekwa katika hali ya tahadhari tangu ianzishe mashambulizi dhidi ya wapiganaji wa Islamic State wa Syria na Wakurdi Kaskazini mwa Iraq.

CAF kumuunga mkono INFANTINO Urais wa FIFA

Shirikisho la soka barani Afrika CAF linamuunga mkono Infantino Rais wa shirikisho la soka barani Africa (CAF) AHMAD AHMAD amesema shir...