Monday, 10 August 2015
Marekani yashambuliwa Uturuki.
Watu wenye silaha wameufyatulia risasi ubalozi wa Marekani katika mji mkuu wa Uturuki, Istanbul.
Watu wawili walitoroka wakati maafisa wa polisi walipowafyatulia risasi lakini ripoti zinasema kuwa mshukiwa mwanamke tayari ametiwa mbaroni.
Hakuna habari zo zote za majeruhi zilizotolewa.
Shambulio hilo lilitokea muda mfupi baada ya bomu kulipuka kwenye gari moja lililokuwa limeegeshwa karibu na kituo cha polisi.
Watu kumi walijeruhiwa, wakiwemo maafisa watano wa polisi.
Inasemekana kuwa washukiwa wawili na afisa mmoja wa polisi walifariki.
Haijulikani iwapo mashambulizi hayo mawili yana uhusiano.
Uturuki imewekwa katika hali ya tahadhari tangu ianzishe mashambulizi dhidi ya wapiganaji wa Islamic State wa Syria na Wakurdi Kaskazini mwa Iraq.
Subscribe to:
Posts (Atom)
CAF kumuunga mkono INFANTINO Urais wa FIFA
Shirikisho la soka barani Afrika CAF linamuunga mkono Infantino Rais wa shirikisho la soka barani Africa (CAF) AHMAD AHMAD amesema shir...

-
Tuzo za VMA 2014 zimefanyika na mastaa wengi walifika kwenye hilo tukio. Listi ya mastaa hao iliongozwa na familia ya Jay Z na Beyon...
-
Luca Modric mchezaji bora wa mwaka wa FIFA Wameamua kumpa,ni baada ya kumdhurumu tuzo yake ya msimu wa 2009/10,mwaka huu wameona ai...
-
Mlinda mlango wa Derby Country akipangua mkwaju wa Phil Jones Timu ya DERBY COUNTY inayonolewa na nyota wa zamani wa CHELSEA, FRANK LAM...