Saturday, 5 September 2015
ugonjwa wa Ebola upya umekua tishio tena Sierra Leone.
Watu 1,000 nchini Sierra Leone wamewekwa kwenye karantini baada ya kugunduliwa kuwa mwanamke wa umri wa miaka 67 alifariki kutokana na Ebola.
Hilo limejiri siku tano tu baada ya kuanza kwa hesabu ya wiki sita iliyolenga kutangaza taifa hilo kuwa bila Ebola.
Karantini hiyo itadumu wiki tatu, mradi tu kusiwe na visa vipya vitakavyoripotiwa.
Watu Zaidi ya 11,000 wamefariki tangu kuanza kwa mkurupuko wa Ebola nchini Sierra Leone, Guinea na Liberia.
Mwandishi wa BBC Umaru Fofana katika mji mkuu wa Freetown, anasema maafisa wa serikali nchini humo walikuwa na matumaini baada ya kupita kwa kipindi kirefu bila kisa kipya cha Ebola na kwamba kisa cha sasa kimewashangaza.
Mwandishi wetu anasema karantini ya sasa ina masharti makali zaidi kuliko za awali. Ni pamoja na amri ya kuzuia watu kutembea kutoka nyumba moja hadi nyingine.
Wanajeshi na maafisa wa polisi wametumwa kudumisha karantini hiyo katika kijiji cha Sellakaffta, kilichoko Kambia kwenye mpaka wa kaskazini wa taifa hilo na Guinea.
Maafisa wa Shirika la Afya Duniani na wizara ya afya Sierra Leone wanapanga kutoa chanjo kwa wale ambao huenda walikutana na mwanamke huyo.
Guinea inajaribu kudhibiti mkurupuko wa ugonjwa huo nchini humo. Liberia, WHO ilitangaza kuwa virusi vya Ebola vimeacha kusambaa kwa mara ya pili Alhamisi.
Taifa hilo lilitangazwa kutokuwa na Ebola mwezi Mei lakini visa zaidi vikaripotiwa mwezi uliofuata.
baada ya huyu mtoto kufariki dunia Baba yake akataa hifadhi,ni huko syria. inauma sana , soma hii
Baba wa mtoto kutoka nchini Syria ambaye alikufa maji wiki hii na kuzua changamoto za kutaka kuchukuliwa hatua za kutatua suala la uhamiaji nchini syria anaripotiwa kukataa hatua ya Canada ya kumpa makao.
Tima Kurd, ambaye ni dadake Abdullah al Kurdi alisema, alimuambia kuwa anataka kusalia nchini Syria yaliko makaburi ya mkewe na wanawe wawili wa kiume ambao pia walikufa maji nje ya pwani ya Uturuki siku ya jumatano.
Wote hao walizikwa nchini Syria siku ya Ijumaa
Picha za mwili wa mtoto huyo wa miaka mitatu katika ufuo wa Uturuki zilizua mjadala kuhusu hatma ya watu wanaokimbia mapigano nchini Syria.
Subscribe to:
Posts (Atom)
CAF kumuunga mkono INFANTINO Urais wa FIFA
Shirikisho la soka barani Afrika CAF linamuunga mkono Infantino Rais wa shirikisho la soka barani Africa (CAF) AHMAD AHMAD amesema shir...

-
Tuzo za VMA 2014 zimefanyika na mastaa wengi walifika kwenye hilo tukio. Listi ya mastaa hao iliongozwa na familia ya Jay Z na Beyon...
-
Luca Modric mchezaji bora wa mwaka wa FIFA Wameamua kumpa,ni baada ya kumdhurumu tuzo yake ya msimu wa 2009/10,mwaka huu wameona ai...
-
Mlinda mlango wa Derby Country akipangua mkwaju wa Phil Jones Timu ya DERBY COUNTY inayonolewa na nyota wa zamani wa CHELSEA, FRANK LAM...