Thursday, 10 September 2015
hatimae Papa Francis arithia na kupitisha sheria ya talaka kwa wakatoliki wote duniani.
kiongozi mkuu wa kanisa katoliki duniani Papa Francis ameridhia talaka kwa ndoa za Waumini wa Kanisa Katoliki na kuruhusu kuoa tena.
hayo yanakuja baada ya changamoto mbalimbali ambazo zilikua zinalikumba kanisa hilo , papa amepitisha sheria hiyo kwa maslahi ya wakatoliki ambao walikua wakipata matatizo ya kindoa bila kupata ufumbuzi kwa miaka mingi na kubakia ndani ya ndoa bila ya upendo wa dhati ambao haumpendezi mungu, hatua hii inatajwa kua ya muhimu na ya kihistoria kufanywa na kiongozi mkubwa kama huyu duniani. kwa taarifa zaidi endelea kuingia innosam.blogspot.com
huko nchini ghana Majaji 34 kizimbani kwa kula rushwa
Uchunguzi
uliofanywa na mwandishi habari za uchunguzi , Anas Aremeyaw Anas
uliomchukua miaka miwili umegundua kuwa majaji pamoja na viongozi wa juu
wa mahakama nchini humo wanakula rushwa .
Anas tayari amekwisha
waandikia waraka Rais wa nchi hiyo pamoja jaji mkuu ambao nao tayari
wamekwisha andaa tume ya kuwahoji majaji wote wanaotuhumiwa.Kwa mjibu wa aliyeitengeneza kanda hiyo yenye urefu wa takribani saa mia tano, ilirekodiwa kwa zaidi ya miaka miwili. Ni majuma mawili sasa tangu Jaji Mkuu wa Ghana alipokabidhiwa nakala yake.
Rekodi hiyo inaonyesha majaji wa mahakama ndogo na za juu wakichukua hongo na kuwalazimisha wenye kesi kutoa pesa.
Anes, Mwandishi wa habari za uchunguzi, ambaye pia ni mwanasheshia aliwafuata majaji kuwapa hongo ili wawaachie huru watuhumiwa. Katika maeneo mengine alijifanya mwenye kushitaki ili atoe hongo. Leo, chombo kinachohusika na kuwaadhibu wanasheria wanaolalamikiwa kwa rushwa kitawasikiliza majaji wote 34 wanaohusishwa na kashifa hiyo.
Tuhuma za rushwa si mpya katika mahakama za nchini Ghana lakini ambacho kimekuwa kikikosekana ni ushahidi madhubuti. Kwa Waghana wengi, uchunguzi huu wa sasa ni ushahidi mzuri wa kuunga mkono malalamiko yao ya muda mrefu juu ya rushwa katika mahakama.
Mwandishi huyo wa habari za uchunguzi anapanga kuiachia video hiyo katika Ukumbi wa Kimataifa wa mikutano wa Ghana mwezi ujao.
Subscribe to:
Posts (Atom)
CAF kumuunga mkono INFANTINO Urais wa FIFA
Shirikisho la soka barani Afrika CAF linamuunga mkono Infantino Rais wa shirikisho la soka barani Africa (CAF) AHMAD AHMAD amesema shir...

-
Tuzo za VMA 2014 zimefanyika na mastaa wengi walifika kwenye hilo tukio. Listi ya mastaa hao iliongozwa na familia ya Jay Z na Beyon...
-
Luca Modric mchezaji bora wa mwaka wa FIFA Wameamua kumpa,ni baada ya kumdhurumu tuzo yake ya msimu wa 2009/10,mwaka huu wameona ai...
-
Mlinda mlango wa Derby Country akipangua mkwaju wa Phil Jones Timu ya DERBY COUNTY inayonolewa na nyota wa zamani wa CHELSEA, FRANK LAM...