Wednesday, 24 June 2015

watu 18 wafa huko china leo


 



Watu wa kabila la Uigurs nchini Uchina
Ripoti za vyombo vya habari nchini Marekani zinasema kuwa watu 18 wameaga dunia katika eneo la Uchina la Xinjiang katika makabiliano na polisi katika eneo la ukaguzi.
Radio Free Asia inasema kuwa watu hao wa kabila la Uighurs walitumia visu na mabomu kuwashambulia maafisa wa polisi.
Hakujakuwa na mawasiliano rasmi kuhusu tukio hilo lakini wafanyikazi wa hospitali katika mji wa Kashgar wameiambia BBC kuwa maafisa hao wa polisi walipokea matibabu.
Moja ya lengo huenda ni kuweka vikwazo vikali kwa waislamu wa Uighurs katika mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadan.

watu 120 wameuwa hivi punde huko mogadishu

 

Mogadishu Somalia





Mlipuaji wa kujitolea muhanga ameligongesha gari lake na lile la kijeshi katika mji mkuu wa Somalia Mogadishu na kusababisha mlipuko mkubwa.

Ripoti zinasema kwamba takriban watu 12 waliuawa na wengine kujeruhiwa wengi wakiwa raia.

Shambulizi hilo lilitokea karibu na ubalozi wa falme za kiarabu UAE
Vyombo vya habari nchini Somalia vimeripoti kwamba balozi amenusurika mlipuko huo ambao umeutaja kama jaribio la mauaji.

CAF kumuunga mkono INFANTINO Urais wa FIFA

Shirikisho la soka barani Afrika CAF linamuunga mkono Infantino Rais wa shirikisho la soka barani Africa (CAF) AHMAD AHMAD amesema shir...