Tuesday, 27 May 2014

MAFURIKO YAITIKISA CHINA , ZAIDI YA  20 WAFARIKI DUNIA .

Screen Shot 2014-05-27 at 2.30.30 AMNi dhoruba kali iliyoleta majonzi Kaskazini mwa China ambako mpaka sasa tayari watu 26 wamefariki na wengine 10 hawajulikani walipo huku vyombo vya usalama na uokoaji vikizidi kutafuta njia ya kuepusha maafa zaidi kutokana na hali ya hewa.
Kwenye eneo la Guangdong ni watu 15 wamefariki toka Jumatano iliyopita na wengine watano hawajulikani walipo kutokana na maafa yaliyosababishwa na mvua kubwa zinazonyesha.
Picha zote hizi unazoziona zimepigwa May 25 2014 ambapo hii inaonyesha moja ya familia kwenye eneo hilo ikipata chakula juu ya maji yaliyojaa nyumbani kwao
Screen Shot 2014-05-27 at 2.30.22 AM
Screen Shot 2014-05-27 at 2.30.10 AM
Screen Shot 2014-05-27 at 2.30.01 AMcredits to millardayo 

 bongo movie wapat pigo jingine pata 

Screen Shot 2014-05-27 at 8.56.46 AMTukiwa na wiki moja toka tumzike muongozaji na muigizaji Adam Kuambiana leo asubuhi imetoka taarifa nyingine ya kifo cha miongoni mwa waigizaji wa kike toka Bongo Movie.
Aliefariki ni mwigizaji anaitwa Rachel Haule ambaye kacheza movie mbalimbali ikiwemo Vanesa in Dilema.
Screen Shot 2014-05-27 at 8.56.59 AMChanzo cha kifo chake chake bado hakijafahamika ingawa taarifa za mwanzo zinasema alikua mjamzito na alikwenda Muhimbili kwa ajili ya kujifungua baadae alifanikiwa kujifungua lakini kwa bahati mbaya mtoto alifariki nae hali ilibadilika akapelekwa ICU lakini baadae akafariki.

CAF kumuunga mkono INFANTINO Urais wa FIFA

Shirikisho la soka barani Afrika CAF linamuunga mkono Infantino Rais wa shirikisho la soka barani Africa (CAF) AHMAD AHMAD amesema shir...