VODACOMA Tanzania ni miongoni mwa
makampuni yaliyojitokeza kudhamini
ziara ya magwiji waliocheza kwa
mafanikio makubwa katika klabu ya
Real Madrid.
Kikosi cha magwiji hao maarufu kama
`Real Madrid Legends` kitafanya ziara
ya siku nne nchini kuanzia Agosti 22
mwaka huu na kitacheza mechi moja
ya kirafiki dhidi ya kikosi maalumu
cha nyota wa Tanzania.
Akizungumza leo na waandishi wa
habari katika hoteli ya New Afrika,
jijini Dar es salaam, meneja wa ziara
hiyo, Dennis Ssebo amesema mbali na
Vodacom, wadhamini wengine ni
Fastjet, Tropical, Pembe Flower, Lake
Gas, EFM Radio na Ladger Plaza Bahari
Beach.
Ziara hiyo ni mwaliko wa kampuni ya
Tanzania Sisi ni Nyumbani (TSN), chini
ya mkurugenzi wake mkuu, Farough
Baghozah na meneja wa ziara hiyo ni
Dennis Ssebo.
Wachezaji wa Real Madrid waliocheza
La Liga miaka ya nyuma, ligi ya
mabingwa kombe la dunia kama vile
Mfaransa Zinedine Zidane, Mreno Luis
Madeila Figo na Mbrazil Ronaldo de
Lima watakuwepo katika ziara hiyo.
Ssebo kabla ya mkutano wa leo,
aliuambia mtandao huu kuwa
maandalizi ya ziara hiyo yanakwenda
vizuri na itakuwa fursa pekee kwa
Watanzania kuiona Real Madrid kwa
mara ya kwanza barani Afrika.
“Ninaloweza Kusema ni kwamba,
Watanzania wakae tayari kupokea
wachezaji 27 wa zamani wa timu ya
Real Madrid na mashabiki 23 kutoka
Hispania wanaokuja kuwashangilia
magwiji wao. Kwahiyo jumla
tunapokea watu 50 kutoka Hispania
kwa ajili ya ziara hii”. Alisema Ssebo.
“Ni ziara ambayo tulifikiria itakuwa
fupi, lakini wenzetu kumbe
wameipenda nchi na wanaifahamu,
kwahiyo ni ziara ambayo itachukua
takribani siku nne”. Aliongeza
Wednesday, 23 July 2014
HII HAPA ILE LIST YA WALE MASTAA WA MADRID WATAOKUJA TANZANIA SOON AS POSSIBLE.
KOCHA MPYA WA BRAZILI ATANGAZWA LEO. Ni yule kipenzi cha wengi
Shirikisho la soka la Brazil CBF,
limemtangaza aliyekuwa mchezaji wa
Brazil, Dunga kuwa kocha wa timu ya taifa
kwa mara ya pili.
Dunga aliyeiongoza Brazil kutwaa kombe
la dunia la mwaka wa 1994 aliwahi pia
kuwa kocha katika mwaka wa 2006 hadi
2011. Dunga amechukua nafasi ya Luiz
Felipe Scolari, ambaye alijiuzulu kufuatia
kimbunga cha mabao 7-1 ambayo timu
hiyo ililazwa na Ujerumani katika hatua ya
nusu fainali .
Scolari mwenye umri wa miaka 65
aliiongoza Brazil katika semi fainali za
kombe la dunia ambapo timu hiyo ilipata
kichapo kibaya cha mabao masaba kwa
moja dhidi ya mabingwa wa kombe la
Dunia Ujerumani.
Dunga amewapiku mkufunzi wa kilabu ya
Corinthians Tite,Mkufunzi wa kilabu ya
Sau Paulo Muriciy Ramalho na Vanderlei
Luxembourg ambaye aliwahi kuifunza
timu hiyo kutoka mwaka 1998 hadi
mwaka 2000.
Wachezaji wanamtaka kocha Sabella
kuiongoza timu hiyo katika kipute cha
kuwania ubingwa wa mataifa ya Amerika
ya Kusini yaani 2015 Copa America
mashindano yatakayoandaliwa huko Chile
CAF kumuunga mkono INFANTINO Urais wa FIFA
Shirikisho la soka barani Afrika CAF linamuunga mkono Infantino Rais wa shirikisho la soka barani Africa (CAF) AHMAD AHMAD amesema shir...

-
Tuzo za VMA 2014 zimefanyika na mastaa wengi walifika kwenye hilo tukio. Listi ya mastaa hao iliongozwa na familia ya Jay Z na Beyon...
-
Luca Modric mchezaji bora wa mwaka wa FIFA Wameamua kumpa,ni baada ya kumdhurumu tuzo yake ya msimu wa 2009/10,mwaka huu wameona ai...
-
Mlinda mlango wa Derby Country akipangua mkwaju wa Phil Jones Timu ya DERBY COUNTY inayonolewa na nyota wa zamani wa CHELSEA, FRANK LAM...