Hii ndoa pia ilishuhudiwa na watoto wao wawili mapacha kama wanavyoonekana kwenye picha pamoja na marafiki wengine wa familia pamoja na ndugu ambao idadi yao inafikia 50.
Monday, 6 April 2015
PAPA MTAKATIFU ATOA SALAMU ZA RAMBI RAMBI KWA WANAFUNZI WALIOFARIKI KENYA.
Katika maadhimisho ya ibada ya sikukuu ya Pasaka, baada ya mateso,kifo na ufufuko wa Yesu Kristo,Baba Mtakatifu Francis amewaombea wanafunzi waliouawa nchini Kenya mwishoni mwa wiki iliyopita.
Katika utaratibu wake wa kawaida wa kutoa ujumbe katika sikukuu ya pasaka,akizungumza na umati wa waumini waliofurika katika viwanja vya Basilica ya Mtakatifu Peter mjini Vatican, Papa ametoa mwito wa kusitisha kile alichokiita matukio mengi ya mateso ya wakristo ulimwenguni.
Kiongozi huyo wa kiroho anayeongoza waumini wa madhehebu ya kikatoliki wapatao bilioni moja nukta mbili ,amelaani mgogoro unaondelea Mashariki ya kati na kwingineko, lakini ameweka imani yake katika mazungumzo yanayoendelea juu ya mkataba wa vinu vya nyukilia vya Irani ,wenye mwanga wa matumaini wa kufikiwa makubaliano na kuifanya dunia kuwa mahali salama pa kuishi.
Kabla ya kuanza hotuba yake,Papa alikwenda katika viwanja hivyo vya Basilica la Mtakatifu Petro kuwasalimia waumini waliokuwa wakimsubiri pamoja na kwamba kulikuwa na hali mbaya ya hewa.
kasi ya watu kujiunga na ugaidi dunia yaongezeka kwa kasi ya ajabu.
Zaidi ya wapiganaji wa kigeni elfu ishirini na watano kutoka mataifa mia moja walisafiri kwa nia na malengo ya kujiunga na makundi ya kijeshi kama al-Qaeda na Islamic State (IS), taarifa ya umoja wa mataifa imeeleza hayo.
Taarifa hiyo imeeleza pia kwamba wapiganaji wageni ulimwenguni idadi yao imeongezeka mpaka kufikia asilimia sabini na moja katikati ya mwaka 2014 na march mwaka huu.
Nchi za Syria na Iraq ndizo nchi zinazolengwa kwa ukaribu zaidi na ndicho kitovu cha vijana wanaomaliza mazomo yao na kugeuka kuwa wenye msimamo mkali wa kidini.
Na pia taarifa hiyo imebainisha kuwa endapo kundi la IS lingeshindwa nchini Syria na Iraq,sasa wapiganaji hao kutoka nchi za kigeni wamesambaa ulimwenguni .
Nalo baraza la usalama la umoja wa mataifa liliwaomba wataalamu wa masula ya kijeshi miezi sita iliyopita kuchunguza vitisho vya askari wa kigeni wanaojiunga na kundi la Is na makundi mengine ya kigaidi.
Katika ripoti iliyowasilishwa kwenye baraza hilo mwishoni mwa mwezi uliopita ,na wataalamu wakaeleza kuwa ongezeko la wapiganaji wa nchi za kigeni zinazidi kuongezeka kulinganisha na muongo mmoja uliopita .
Maelfu ya wapiganaji wa kigeni ambao hufanya safari hadi nchini Syria ,Falme za Kiarabu na Iraq huko hufanya makao na kufanya kazi na kumalizia masomo ya elimu ya juu kwa wenye msimamo mkali kamalivyowahi kutokea kwatika nchi ya Afghanistan miaka ya 1990 .
Syria na Iraq inasemekana ina makaazi elfu ishirini na mbili kwa wapiganaji hao wa kigeni ,pia nchini Afghanistan makaazi elfu sita na mia tano na maelfu ya makaazi nchini Yemen, Libya, Pakistan na Somalia.
Shambulizi Garissa:Serikali ya kenya yajitetea yajitetea
Serikali ya Kenya imeitetea idara yake ya usalama kufuatia shutma kwamba ilichelewa kukabiliana na shambulio la chuo kikuu cha Garissa ambapo takriban watu 150 waliuawa.
Shambulio hilo lilisitishwa baada wapiganaji wanne waliohusika kuuawa na maafisa wa polisi saa 15 baada ya kuvamia chuo hicho.
Lakini naibu wa rais William Ruto anasema kuwa kundi la kwanza la polisi liliwasili katika chuo hicho saa moja baada ya shambulizi.
Amelipongeza jeshi la Kenya KDF kwa kile alichokitaja kua hatua za haraka.Lakini vyombo vya habari vimekuwa vikisema kuwa vikosi maalum vilivyowaua wapiganaji hao vilichelewa kufika katika eneo hilo kutokana na mfumo wa usafiri waliotumia.
Pia kuna madai kwamba maafisa wa polisi walifeli kuchukua hatua za dharura baada ya kupewa habari kwamba mmoja ya wauaji ambaye sasa ametambuliwa kama Abdirahim Abdullahi ni wakili na mwana wa chifu mmoja katika eneo la kazkazini mashariki.
Subscribe to:
Posts (Atom)
CAF kumuunga mkono INFANTINO Urais wa FIFA
Shirikisho la soka barani Afrika CAF linamuunga mkono Infantino Rais wa shirikisho la soka barani Africa (CAF) AHMAD AHMAD amesema shir...

-
Tuzo za VMA 2014 zimefanyika na mastaa wengi walifika kwenye hilo tukio. Listi ya mastaa hao iliongozwa na familia ya Jay Z na Beyon...
-
Luca Modric mchezaji bora wa mwaka wa FIFA Wameamua kumpa,ni baada ya kumdhurumu tuzo yake ya msimu wa 2009/10,mwaka huu wameona ai...
-
Mlinda mlango wa Derby Country akipangua mkwaju wa Phil Jones Timu ya DERBY COUNTY inayonolewa na nyota wa zamani wa CHELSEA, FRANK LAM...