Sunday, 17 January 2016

star tv , radio free africa na kiss fm zafungiwa kuruka hewani na TCRA ,soma sababu hapa.

Image captionTCRA
Mamlaka ya mawasiliano nchini Tanzania, TCRA imevifungia vituo vya Radio na Television kwa muda wa miezi 3 kikiwemo kituo cha Star TV, Radio free Afrika, Kiss Fm na Uhuru FM.
Vituo hivyo vimefungiwa kutoa huduma kwa miezi mitatu kila moja baada ya kushindwa kulipa kodi
Kulingana na mtandao wa jamii Forum,mnamo mwezi July 2015 Serikali ilitoa taarifa kwa umma na TCRA kwamba baadhi ya radio na Televisheni zipatazo 40 zinadaiwa ada na tozo mbalimbali.
Aidha Serikali iliviagiza vituo hivyo kuhakikisha kuwa vimelipa ada kufikia tarehe 31 mwezi Disemba 2015.
Hatahivyo baadhi ya vituo hivyo vililipa kodi hiyo mwanzoni mwa mwezi huu na wengine wakishindwa kulipa.
Kwa mujibu wa sheria unaposhindwa kulipa kodi TCRA huchukulia kwamba haupo.
TCRA sasa inasema kuwa iwapo miezi mitatu ijayo itakamilika bila malipo hayo kufanywa basi italazimika kuchukua hatua zaidi kama vile kuwapokonya leseni wahusika.
Ni vituo 11pekee kati ya vituo vilivyokuwa vikidaiwa na mamlaka hiyo vilivyotiii agizo hilo na kulipa.
Baadhi ya vituo hivyo ambavyo havitakuwa hewani kufikia jumatatu ni
1. Sibuka FM 2. Breez FM 3. Country FM 4. Ebony FM 5. Hot FM 6. Impact FM 7. Iringa Municipal TV 8. Kiss FM 9. Kitulo FM 10. Kifimbo FM 11. Mbeya City Municipal TV 12. Radio 5 13. Radio Free Afrika (RFA) 14. Musa Television Network 15. Pride FM radio 16. Radio Huruma 17. Radio Uhuru 18. Star TV 19. Rock FM Radio 20. Standard FM radio 21. Sumbawanga Municipal TV 22. Tanga City TV 23. Top Radio FM limited 24. Ulanga FM

mbwana Samatta apewa zawadi nono na serikali ya Tanzania, soma na itazame zawadi hiyo hapa




Samatta
Image captionSamatta aliibuka mfungaji mabao bora ligi ya klabu bingwa Afrika 2015

Mchezaji bora wa Afrika kwa wachezaji wa nyumbani Mbwana Samatta amekabidhiwa sehemu ya ardhi na serikali ya Tanzania kufuatia uhodari wake uliomwezesha kuondoka na tuzo hiyo na kuisaidia TP Mazembe kutwaa kombe la vilabu bingwa Afrika.
Mchezaji huyo pia alitunukiwa zawadi nyinginezo kwenye hafla iliyoandaliwa ili kusherekea mafanikio yake katika soka yaliyoiweka Tanzania katika ramani ya soka.
Hafla hiyo pia ilihudhuriwa na wadau wa michezo nchini Tazania wakiwemo waziri wa michezo Nape Nnauye na Thomas Ulimwengu ambaye ni mchezaji mwenza wa Samatta.
Amepewa kipande cha ardhi eneo la Kigamboni, Dar es Salaam na serikali kupitia wizara ya ardhi na nyumba.









Mchezaji huyo pia ameteuliwa nahodha mpya wa timu ya taifa Taifa Stars, nafasi ambayo awali ilishikiliwa na beki Nadir Haroub ‘Cannavaro’ anayeichezea klabu ya Yanga, kwa mujibu wa gazeti la Mwananchi.
Samatta, maarufu ‘Samagoal’ aliwapiku Robert Kadiaba na Bounedjah Baghdad wa Algeria anayeichezea klabu ya Etoile du Sahel na kutwaa tuzo hiyo.
Baada ya kupokea taji lake katika sherehe za kuwatuza wachezaji bora Afrika, mjini Abuja, Samatta alirejea Tanzania na baadaye kualikwa na Rais wa Zamani wa Tanzania Jakaya Kikwete.
Mnamo mwaka wa 2013, serikali ya Nigeria iliwakabidhi wachezaji wake sehemu ya ardhi mjini Abuja na pesa kwa kushinda kombe la Afcon.

Watu 21 wauawa nchini Burkina faso katika shambulizi la kushtukiza.ni siku chache baada ya kumpata raisi mpya.



Image copyrightAP
Image captionBurkina faso
Rais wa Burkina Faso amesema takriban watu 21 wameuwawa katika shambulio kwenye hoteli moja mjini Ogadugu na wanamgambo waliovamia hotel hiyo.
Roch Mark Christian Kabore amesema washambuliaji wanne waliovamia hotel hiyo waliuliwa ambapo wawili kati yao ni wanawake. Shambulio hilo lililotokea kwenye hotel ya Splendide kwenye mji mkuu wa Ouagadougou sasa limemalizwa.
Image copyrightAFP GETTY
Image captionbaadhi ya manusura
Waziri wa Ulinzi wa nchi hiyo amesema wanamgambo hao wameuwa watu kumi na nane kutoka mataifa mbalimbali. Zaidi ya watu mia moja na ishirini walikimbia hotel hiyo maarufu kwa watalii.
walionusurika wanasema wanamgambo hao walianza kupiga risasi kwenye jengo hilo na kisha kuliwasha moto.
Image copyrightReuters
Image captionWanajeshi maalum wa ufaransa
Kundi la Kigaidi la Al Qaeda kwenye ukingo eneo jangwa imesema lina husika na shambulio hilo.
Watu 126 waliokuwa mateka waliachiliwa huru katika hoteli ya Splendid iliopo katika mji mkuu wa taifa hilo la Magharibi mwa Afrika Ouagadougou, kwa mujibu wa waziri wa maswala ya ndani.
Image copyrightAP
Image captionEneo lililo karibu na jhoteli ya Splendid ilioshambuliwa
Wapiganaji wanne waliuawa aliongezea huku watu 21 wa mataifa 18 tofauti wakifariki wakati wa shambulio ambalo pia liliulenga mgahawa huo.
Vikosi maalum vya Ufaransa vinasaidia wanajeshi wa taifa hilo katika oparesheni hiyo.
Image captionEneo lililoshambuliwa
Rais wa Ufaransa Francois Hollande ameshtumu shambulio hilo la taifa hilo ambalo lilikuwa koloni yake hapo zamani.
Kundi la Al-Qaeda la islamic Maghreb{AQIM} limesema kuwa lilitekeleza shambulio hilo katika taifa hilo la Magharibi mwa Afrika.
Image captionHoteli ya Splendid
Mnamo mwezi Novemba shambulio la AQIM katika hoteli moja ya Bamako nchini Mali liliwauwa watu 19.

CAF kumuunga mkono INFANTINO Urais wa FIFA

Shirikisho la soka barani Afrika CAF linamuunga mkono Infantino Rais wa shirikisho la soka barani Africa (CAF) AHMAD AHMAD amesema shir...