Tuesday, 10 May 2016

Taharuki: ghorofa kubwa laporomoka huko Mombasa kenya.

Jumba

Image captionMaafisa wa serikali wamefika eneo hilo
Sehemu ya jumba kubwa la kibiashara mjini Mombasa imeporomoka siku chache baada ya jumba la makazi kuporomoka jijini Nairobi na kusababisha vifo vya watu zaidi ya 40.
Sehemu ya jumba hilo la Nyali Centre, yenye ghorofa sita, iliporomoka usiku wa kuamkia Jumatatu.
Hakuna aliyeripotiwa kujeruhiwa wakati wa mkasa huo.
Jumba la Nyali Centre huwa na kituo cha mazoezi na mgahawa maarufu.
Waziri wa serikali ya jimbo la Mombasa Francis Thoya amesema jumba hilo litachunguzwa kubaini iwapo ni thabiti.
“Nadhani sehemu ambapo vyoo hivyo vilifaa kuuunganishwa na jumba lenyewe ndiyo ilikuwa na shida. Ninamsaka mhandisi na aliyepewa kandarasi,” amesema.
“Lakini unapopata visa kama hivi, ni ishara tosha kuwa inafaa tuchunguze upya mijengo yetu. Kwa hivyo kutakuwa na ukaguzi wa baadhi ya mijengo mikuu ambayo inatumiwa na umma.”

Taharuki: ghorofa kubwa laporomoka huko Mombasa kenya.

Jumba

Image captionMaafisa wa serikali wamefika eneo hilo
Sehemu ya jumba kubwa la kibiashara mjini Mombasa imeporomoka siku chache baada ya jumba la makazi kuporomoka jijini Nairobi na kusababisha vifo vya watu zaidi ya 40.
Sehemu ya jumba hilo la Nyali Centre, yenye ghorofa sita, iliporomoka usiku wa kuamkia Jumatatu.
Hakuna aliyeripotiwa kujeruhiwa wakati wa mkasa huo.
Jumba la Nyali Centre huwa na kituo cha mazoezi na mgahawa maarufu.
Waziri wa serikali ya jimbo la Mombasa Francis Thoya amesema jumba hilo litachunguzwa kubaini iwapo ni thabiti.
“Nadhani sehemu ambapo vyoo hivyo vilifaa kuuunganishwa na jumba lenyewe ndiyo ilikuwa na shida. Ninamsaka mhandisi na aliyepewa kandarasi,” amesema.
“Lakini unapopata visa kama hivi, ni ishara tosha kuwa inafaa tuchunguze upya mijengo yetu. Kwa hivyo kutakuwa na ukaguzi wa baadhi ya mijengo mikuu ambayo inatumiwa na umma.”

Pigo Kubwa kwa IS: Kiongozi ‘muhimu’ wa Islamic State auawa

Waheeb


Image copyrightAFP
Image captionAbu Waheeb wakati mwingine alifahamika kama Shakir Waheeb
Jeshi la Marekani limesema mmoja wa viongozi wakuu wa kundi linalojiita Islamic State ameuawa kwenye shambulio la kutoka angani.
Msemaji wa Pentagon Peter Cook amesema Abu Waheeb, ambaye amekuwa afisa mkuu wa kijeshi wa Islamic State katika mkoa wa Anbar nchini Iraq aliuawa pamoja na watu wengine watatu baada ya gari lao kushambuliwa katika eneo la Rutba.
Marekani imesema kifo cha Abu Waheeb ni pigo kubwa kwa uongozi wa IS.
Wahib alizaliwa 1986 na alikuwa mwanafunzi wa zamani wa sayansi ya kompyuta ambaye alielezwa na mitandao inayofuatilia shughuli za Islamic State kama mtu ambaye nyota yake katika kundi hilo ilikuwa iking’aa.
Alikamatwa na wanajeshi wa Marekani nchini Iraq na kuhukumiwa kifo lakini akatoroka jela mwaka 2012.
Mwaka uliofuata, alishiriki katika mauaji ya kundi la madereva wa malori kutoka Syria yaliyokuwa yakipitia Iraq.

CAF kumuunga mkono INFANTINO Urais wa FIFA

Shirikisho la soka barani Afrika CAF linamuunga mkono Infantino Rais wa shirikisho la soka barani Africa (CAF) AHMAD AHMAD amesema shir...