Tuesday, 12 April 2016

majonzi: Mchezaji wa Uingereza auawa nchini Trinidad


Image caption Adrian St John
Mchezaji chipukizi wa Kriketi raia wa Uingereza amefariki baada ya kuripotiwa kupigwa risasi na majambazi nchini Trinidad.
Adrian St John , mwenye umri wa miaka 22 ambaye alikichezea chuo cha mafunzo cha Chris Gayle mjini London anaaminika kufariki siku ya Jumapili.
Mchezaji wa kriketi wa West Indies Gayle alichapisha ujumbe kwenye mtandao wa Twitter akisema " Ni habari mbaya kusikia ,Rambirambi zangu kwa familia na marafiki." Adrian St. John alikuwa nahodha katika chuo hicho.

Image caption Aliuwa baada ya kusimamisha gari lake ili kuwachukuwa rafiki zake alipovamiwa na kupigwa risasi
Ofisi ya maswala ya mambo ya nchi za kigeni imesema walikuwa kwney mazugumzo na maafisa nchini Trinidad kufuatia kifo cha raia huyo wa Uingereza.
Vyombo vya habari nchini humo vimeripoti kwamba Bwana St.John, alivamiwa baada ya kusimamisha gari lake ili kuwachukuwa rafiki zake alipovamiwa na kupigwa risasi.

hatua mbaya kwa wasomi wa elimu ya juu Wanafunzi 62 wafukuzwa chuoni Nairobi.



Image caption Chuo cha Nairobi kilikumbwa na ghasia zilizotokana na uchaguzi wa viongozi wa wanafunzi.
Jumla ya wanafunzi 62 wa chuo kikuu cha Nairobi nchini Kenya wamefukuzwa kutoka chuo hicho, baada ya kushuhudiwa ghasia zilizosababisa kufungwa kwa chuo kwa muda usio julikana wiki moja iliyopita.
Wanafunzi waliteketeza kwa moto afisi za chuo hicho kutokana na kile kinachotajwa kuwa matokeo ya uchaguzi wa kumchagua kiongozi wa wanafunzi chuoni.
Chuo kikuu cha Nairobi kiliseme kuwa kilichukua hatua hizo za kinidhamu dhidi ya wanafunzi walioshiriki katika kuharibu mali ya umma.

CAF kumuunga mkono INFANTINO Urais wa FIFA

Shirikisho la soka barani Afrika CAF linamuunga mkono Infantino Rais wa shirikisho la soka barani Africa (CAF) AHMAD AHMAD amesema shir...