Saturday, 13 June 2015
miss tanzania siti mtemvu alievuliwa taji nusura ajiue mwenyewe .atoa tamko zito.
Aliyekuwa Miss Tanzania 2014, Sitti Mtemvu
aliyeamua kulitema taji hilo baada ya kubebeshwa kashfa amesema kuna
wakati alitaka kujiua lakini alirudisha moyo nyuma na kuona ingekuwa
shida kubwa nyumbani kwao.
“Sikuwa na
amani, niliishi maisha ya hofu, kujifungia ndani, kulia wakati wote.
Ilifikia hatua baba yangu alipata mshktuko kiasi cha kwenda kutibiwa
Afrika Kusini. Mama yangu pia alipata mshtuko…ningeweza kumpoteza.”—Sitti Mtemvu.
“Mama
yangu alisali na mimi, alinipigania, hakuonyesha hadharani jinsi gani
anaumia, lakini ukweli ni kwamba nilimwona alivyokuwa anadhoofu na
kukosa raha. Nyumba yetu iligeuka sehemu ya huzuni, amani ilitoweka ni
kama tulikuwa na msiba.”—Sitti Mtemvu.
Sitti anasema siku moja mama yake alimwambia kwamba aliumia siku alipompoteza mama yake lakini machungu aliyoyasikia kwa Sitti ni mazito zaidi japo baba yake wakati wote alivumilia na hakuonesha maumivu yake.
Anasema kuna wakati baba yake alikwenda
Afrika Kusini na akiwa huko alimtumia ujumbe wa kumuomba msamaha na
alimwambia kwamba hizo ni changamoto.
Sitti anasema alikuwa katika wakati mgumu kiasi cha kufikia uamuzi wa kutupa laini yake ya simu ya zamani.
hii hapa jinsi ya kutazama live tuzo za kili music zinavyoendelea kusherekewa hivi sasa na kutolea hapa mlimani city
Zimebaki saa chache tu kushuhudia
historia nyingine kwenye Industry ya Muziki Tanzania ikiandikwa.. Jana
JUNE 12 2015 ulitangazwa utaratibu mpya ambapo tofauti na miaka ya
nyuma, safari hii zimetolewa Kadi Maalum za Mwaliko kwa wageni wote
watakaoingia pale Ukumbi wa Mlimani City.
Haimaanishi kwamba ulie nyumbani ndio
umepitwa, Clouds TV itakuwa ikirusha Live.. lakini pia urahisi mwingine
ni huu, kuna hii link hapa ambayo ukiibonyeza itakupa nafasi na wewe
kushuhudia LIVE popote ulipo hata kwa kifaa kama simu ya mkononi
>>>http://livestream.com/accounts/4180642/events/4119876/player?width=960&height=540&autoPlay=true&mute=false
kuelekea kili music awards leo usiku ,haya ndio mabadiliko yaliyotokea hivi punde.
Leo June 12 2015 tunahesabu saa chache tu kushuhudia Historia ikiandikwa kwenye Burudani ya Muziki TZ, Tuzo kubwa za Muziki Tanzania, KTMA 2015 leo kuna kipya kilichotangazwa na waandaaji wa Tuzo hizo.
“Kuna mabadiliko machache tofauti na ilivyokuwa mwaka jana… tumebadilisha mpangilio wa Venue ambao kwa mwonekano watu wote wataangalia mbele… mbali na hayo baada ya Show tumeandaa sherehe ambayo itawajumuisha watu wote kuburudika kwa pamoja tofauti na kipindi kilichopita“>>> Pamela Kikuli
“Pia tofauti iliyopo ni kwamba hakutakuwa na utaratibu wa watu kulipia na kuingia kwenye show badala yake watahudhuria wale ambao wamepokea mwaliko tu“>>>
“Tumeona sio vibaya kupokea maoni kutoka kwa wadau mbali mbali ambao wanafuatilia Show hizi ndio sababu iliyotufanya tufanye mabadiliko makubwa kwenye show hii kwa mwaka 2015“>>> Pamela Kikuli.
Sauti ya Pamela Kikuli iko hapa.
ray c alia machozi leo bila msaada wowote. inasikitisha sana, muone na ujue kilichompata
“Nashindwa kuvumilia, niko hapa kitengo cha madawa. Mpaka sasa hivi sijapewa dawa, kwa sababu nilipost ile post nyingine wananifanyia kama makusudi.. Nikikosa dawa wanataka nirudi kuvuta unga?
Wana maamuzi yao lakini unakuta mtu umechelewa kama mimi natoka Bunju kila siku lazima niweke mafuta ya elfu 30 unawaambia nina tatizo bado ukifika unaambiwa imekuwa kama shule“
Ile dawa inauma.. Mwili unauma nasikia baridi mifupa inauma.. alafu wanajua lakini wanatunyima“
Korea Kusini yakumbwa na ugonjwa wa homa ya ajabu sana.soma hii
Shirika
la afya duniani WHO linasema kuwa mlipuko wa homa ya Middle East
Respiratory Syndrome au MERS nchini Korea Kusini na mkubwa na huenda
kesi zaidi zikaripotiwa.
Baada ya uchunguzi wa wiki moja shirika
la WHO linasema kuwa madaktari nchini korea kusini ambao hawakuhufahamu
ugonjwa huo huenda walichangia ugonjwa usambae kwa haraka .Utawala nchini korea kusini unasema kuwa watu 12 wameambukizwa ugonjwa wa MERS huku 14 wakijulikana kuaga dunia.
Subscribe to:
Posts (Atom)
CAF kumuunga mkono INFANTINO Urais wa FIFA
Shirikisho la soka barani Afrika CAF linamuunga mkono Infantino Rais wa shirikisho la soka barani Africa (CAF) AHMAD AHMAD amesema shir...

-
Tuzo za VMA 2014 zimefanyika na mastaa wengi walifika kwenye hilo tukio. Listi ya mastaa hao iliongozwa na familia ya Jay Z na Beyon...
-
Luca Modric mchezaji bora wa mwaka wa FIFA Wameamua kumpa,ni baada ya kumdhurumu tuzo yake ya msimu wa 2009/10,mwaka huu wameona ai...
-
Mlinda mlango wa Derby Country akipangua mkwaju wa Phil Jones Timu ya DERBY COUNTY inayonolewa na nyota wa zamani wa CHELSEA, FRANK LAM...