Aliyekuwa Miss Tanzania 2014, Sitti Mtemvu
aliyeamua kulitema taji hilo baada ya kubebeshwa kashfa amesema kuna
wakati alitaka kujiua lakini alirudisha moyo nyuma na kuona ingekuwa
shida kubwa nyumbani kwao.
“Sikuwa na
amani, niliishi maisha ya hofu, kujifungia ndani, kulia wakati wote.
Ilifikia hatua baba yangu alipata mshktuko kiasi cha kwenda kutibiwa
Afrika Kusini. Mama yangu pia alipata mshtuko…ningeweza kumpoteza.”—Sitti Mtemvu.
“Mama
yangu alisali na mimi, alinipigania, hakuonyesha hadharani jinsi gani
anaumia, lakini ukweli ni kwamba nilimwona alivyokuwa anadhoofu na
kukosa raha. Nyumba yetu iligeuka sehemu ya huzuni, amani ilitoweka ni
kama tulikuwa na msiba.”—Sitti Mtemvu.
Sitti anasema siku moja mama yake alimwambia kwamba aliumia siku alipompoteza mama yake lakini machungu aliyoyasikia kwa Sitti ni mazito zaidi japo baba yake wakati wote alivumilia na hakuonesha maumivu yake.
Anasema kuna wakati baba yake alikwenda
Afrika Kusini na akiwa huko alimtumia ujumbe wa kumuomba msamaha na
alimwambia kwamba hizo ni changamoto.
Sitti anasema alikuwa katika wakati mgumu kiasi cha kufikia uamuzi wa kutupa laini yake ya simu ya zamani.
No comments:
Post a Comment