Monday, 2 May 2016
Miili ya waliotoweka na kupotea miaka 16 iliyopita yapatikana
Miili ya wakwea milima wawili kutoka Marekani waliotoweka katika milima ya Himalaya miaka 16 iliyopita imepatikana.
Mkwea
milima maarufu duniani Alex Lowe alikuwa akikwea katika kilele cha
Shishapangma chenye urefu wa 8,013m (26,290ft) eneo la Tibet Oktoba 1999
akiwa na mpiga picha David Bridges mkasa ulipotokea.Wawili hao walifukiwa na maporomoko ya theluji.
Miili yao ilionekana na wakwea milima wawili wiki iliyopita ikiwa bado imekwama kwenye theluji.
Yeye na Bridges, 29, walikuwa marafiki wakuu na walikuwa wakitafuta njia mpya ya kukwea mlima Shishapangma , mlima wa 14 kwa urefu duniani.
Mkewe Lowe, Jennifer Lowe-Anker, amesema kupatikana kwa mwili wa mumewe kutasaidia familia yake kutulia.
Jennifer baadaye aliolewa na Conrad Anker mwaka 2001.
Baadaye, yeye na wenzake wengine walitafuta wawili hao kwa siku nyingi bila mafanikio.
Maelfu ya watu watarajiwa kujitokeza kumuaga Papa Wemba.
Maelfu ya watu wanatarajiwa kujitokeza leo mjini Kinshasa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kutoa heshima zao za mwisho kwa mwanamuziki mashuhuri wa nyimbo za rumba Papa Wemba.
Leo ndiyo ni siku ya kwanza ya kipindi cha siku tatu za maombolezo rasmi ya kumuenzi mwanamuziki huyo nchini humo.
Wemba, 66, aliyesifika kote duniani kama mmoja wa wanamuziki nguli wa nyimbo za rumba kutoka DR Congo, alifariki baada ya kuzirai akitumbuiza mjini Abidjanwiki moja iliyopita.
Alipendwa sana na mashabiki kwa nyimbo zake na pia mtindo wake wa mavazi.
Mwanamuziki huyo, ambaye jina lake la kuzaliwa ni Jules Shungu Wembadio Pene Kikumba, anatarajiwa kuzikwa Jumatano.
Rais Joseph Kabila ni miongoni mwa wanaotarajiwa kuhudhuria ibada ya wafu leo kwa heshima ya marehemu mjini Kinshasa.
Subscribe to:
Posts (Atom)
CAF kumuunga mkono INFANTINO Urais wa FIFA
Shirikisho la soka barani Afrika CAF linamuunga mkono Infantino Rais wa shirikisho la soka barani Africa (CAF) AHMAD AHMAD amesema shir...
-
Image caption Uganda haipaswi kuzuia upinzani, Obasanjo Aliyekuwa rais wa zamani wa Nigeria, Olusegun Obasanjo, ametaka pande zote pinza...
-
Tuzo za VMA 2014 zimefanyika na mastaa wengi walifika kwenye hilo tukio. Listi ya mastaa hao iliongozwa na familia ya Jay Z na Beyon...