Wednesday, 3 June 2015

kama hukuona lile gari ya kifahari liliyokua linahusishwa na escrow lione hapa. ni shidaaaaaaa


B7k1IiDIQAA0pUg
Rolls Dude
 Hapa tayari iko barabarani na namba za usajili wa Kenya.
rolls_r
rolls2
Rollls
Hii ndi

Blatter ajiuzulu , soma hii kuhusu soccer duniani


Sepp Blatter ameutingisha ulimwengu wa soka hapo jana kwa kusema kwamba anajiuzulu akiwa kama Rais wa Shirikisho la Sola la Kimataifa FIFA kutokana na uchunguzi wa rushwa ambao hivi sasa unamjumuisha hata kiongozi huyo mwenyewe binafsi mwenye umri wa miaka 79. Mtu aliezungumza kwa sharti la kutotajwa jina ameliambia shirika la habari la Uingereza Reuters hapo jana kwamba Blatter ambaye ameliongoza shirika hilo linalosimamia soka duniani tokea mwaka 1998 anachunguzwa na waendesha mashtaka wa Marekani na shirika la upepelezi nchini humo FBI. Msemaji wa FBI amekataa kulizungumzia suala hilo.Blatter raia wa Uswisi ambaye alikuwa ni mtu mwenye ushawishi mkubwa kwenye FIFA kwa miongo mingi ametangaza uamuzi wake wa kujiuzulu katika mkutano na waandishi wa habari ulioitishwa kwa haraka mjini Zurich hapo jana ikiwa ni siku sita baada ya polisi kuivamia hoteli moja mjini humo na kuwakamata maafisa kadhaa wa FIFA na ni siku nne baada ya kuchaguliwa tena kwa muhula wa tano akiwa rais wa FIFA. Amesema uchaguzi wa rais mpya wa FIFA utafanyika karibuni kadri inayowezekana lakini afisa mmoja wa FIFA amesema iwapo uchaguzi huo utafanyika mapema basi itakuwa mwezi wa Disemba.

tambi za kupika kutoka india zakutwa na madini ambayo si salama.soma hapa ujue kama na wewe hua unatumia hii aina ya tambi ili uache

Tambi zapatikana na madini hatari India

Maggy noodles
Maafisa wa mjini Delhi huko India wamepiga marufuku chakula aina ya tambi ziitwazo ''Maggi noodles'' baada ya kufanyiwa uchunguzi na kugunduliwa kuwa na kiwango kikubwa cha madini hatari aina ya lead.
Tambi hizo za ''Maggi noodles'', ambazo zinatengenezwa na kampuni maarufu ya Nestle ya huko India zilikuwa zikipendwa sana na kununuliwa kwa wingi na walaji wengi .

Kampuni yenyewe imejitetea kuwa vyakula vyao ni salama.
Lakini kufuatia tukio hilo la kupigwa marufuku kwa ''Maggi noodles'' hisa zao zimeporomoka katika soko lao la huko India .

idadi kubwa ya tembo yatoweka tanzania. soma hii ni muhimu kuliko.

hii inasababishwa na uwindaji haramu unaofanywa na baadhi ya watanzania , tunaomba ujangili huu ukomeshwe haraka sana kwa ajili ya kuzidi kuhifadhi mali asili ya nchi ambayo ni manufaa kwa kizazi kijacho kama tulivyoikuta sisi baada ya ulindwaji mzuri wa wazee wetu waliotutangulia.



Wanaharakati wa wanyamapori wameelezea hali ya kutoweka kwa idadi ya ndovu kwa asilimia sitini nchini Tanzania katika kipindi cha miaka mitano iliyopita kama janga.
Kundi linalofuatilia maisha ya wanyamapori, TRAFFIC, linasema idadi hiyo inaashiria kiwango halisi cha uwindaji haramu.
Waziri katika serikali ya Tanzania Lazaro Nyalandu, amesema kuwa tatizo hilo lipo kwa kiwango tofauti nchini humo, akitoa mfano kuwa eneo la Serengeti idadi yao inaongezeka .

idadi kubwa ya tembo yatoweka tanzania . soma hapa .piga vita ujangili


Wanaharakati wa wanyamapori wameelezea hali ya kutoweka kwa idadi ya ndovu kwa asilimia sitini nchini Tanzania katika kipindi cha miaka mitano iliyopita kama janga.
Kundi linalofuatilia maisha ya wanyamapori, TRAFFIC, linasema idadi hiyo inaashiria kiwango halisi cha uwindaji haramu.
Waziri katika serikali ya Tanzania Lazaro Nyalandu, amesema kuwa tatizo hilo lipo kwa kiwango tofauti nchini humo, akitoa mfano kuwa eneo la Serengeti idadi yao inaongezeka .

CAF kumuunga mkono INFANTINO Urais wa FIFA

Shirikisho la soka barani Afrika CAF linamuunga mkono Infantino Rais wa shirikisho la soka barani Africa (CAF) AHMAD AHMAD amesema shir...