Tuesday, 25 September 2018

MUPE,MURUKEE,MUPEE,MURUKEEE,MURUKEEEE......!!!!!!



Luca Modric mchezaji bora wa mwaka wa FIFA
Wameamua kumpa,ni baada ya kumdhurumu tuzo yake ya msimu wa 2009/10,mwaka huu wameona aibu.
Labda walimruka kwa makusudi ili watengeneze ushindani wa Lionel Messi na Cristiano Ronaldo uliodumu kwa miaka kumi.

Alikuwa kwenye kiwango bora kabisa cha kuweza kutwaa tuzo ya mchezaji bora wa dunia,lakini kwa kuwa jina lake lilikuwa haliuzi kutokana na klabu na ligi aliyokuwa akiichezea kwa wakati huo,wakaamua kumnyima kwa makusudi"a world is not fair at all"(dunia haina usawa kabisa).

Kitita cha Euro milion 15 (€15m) kilimng'oa Estadio Santiago Bernabeu na kuelekea Giuseppe Meazza kule jijini Milan kumpisha mfalme wa Rossoneri,aliyeacha alama kwenye dimba la San Siro,Ricardo Izecson Dos Santos Leite,Kakà.

Hakukawia kuingia kwenye mfumo wa Jose Mourinho.Nguvu ,stamina na nishati yake uwanjani vilimtofautisha na wachezaji wengi wa nafasi yake uwanjani,akiigawa mipira kwa staili anayoitaka yeye,yaan "mupe,murukee,mupee,murukee,murukee,mupeeee" kama muhudumu wa bar anayewahudumia wateja wake.
Ricardo Kaka mwanasoka bora duniani mwaka 2007

Wesley Benjamin Sneijder,mchezaji wa kimataifa wa Uholanzi aliyemnyima usingizi babu Sir Alex Ferguson wakati wa siku za neema za Manchester United,akiisaka sahihi yake usiku na mchana bila mafanikio.

Msimu wake wa kwanza kutua "Nerazzuri" ,aliisaidia Inter Milan kuchukua makombe makubwa matatu waliyoshiriki.Walichukua ubingwa wa ligi kuu nchini Italia "Serie A" maarufu kama Scudetto,walichukua kombe la Coppa Italia na kisha wakachukua ubingwa wa klabu bingwa barani Ulaya (UCL).

Katika nusu fainali ya klabu bingwa barani Ulaya,Inter Milan walikutana na mabingwa watetezi FC Barcelona,Sneijder aliwaonesha "Italian Job" viungo wa Barcelona waliounda sambusa yao iliyowekwa nta na Lionel Messi,Xavi Hernandez na Andres Iniesta huku Sergio Busquet akiishikilia vyema isianguke na kuingia mchanga.Matokeo ya jumla ya michezo yote miwili,Inter Milan aliingia fainali kwa jumla ya magoli 3-2.

Fainali ikapigwa Santiago Bernabeu,maskani ya pepo ya Sneijder iliyogeuka jehanamu kwake kutokana na ujio wa "Magalacticos " kama Cristiano Ronaldo na Ricardo Kaká.

Sneijder kama kawaida yake awapo uwanjani,akawa anatawanya mipira kuwalisha Diego Milito na Samuel Eto'o kwa mtindo ule ule wa MUPE,MURUKEE,MUPEE,MURUKEE,MURUKEE.Inter Milan wakawafunga Bayern Munich magoli 2-0 huku Sneijder akitoa "assist" moja kati ya magoli hayo yaliyofungwa na Diego Milito.

Wesley Sneijder licha ya kucheza kwenye kiwango cha juu sana hakuwahi kushinda tuzo

Sneijder akatua bondeni kwenye kombe la dunia,akaendeleza wimbi lake la kutawala eneo la kati,safari hii sio kuisaidia timu yake kufuzu kwa kushinda mechi zote nane za makundi,bali aliwapitisha salama kwenye bonde la uvuli na mauti ya soka kwa kuwafungia magoli matano kwenye michuano hiyo,mawili yakiwa dhidi ya "Selecao wa Brazil",na kumaliza mashindano wakiwa washindi wa pili na yeye kuwa na idadi sawa ya magoli na Thomas Müller,mfungaji bora wa Mashindano hayo.

Wakati yanatajwa majina matatu ya wachezaji wanaowania tuzo ya mchezaji bora wa FIFA wa dunia (Ballon d'Or) kipindi hicho,jina la kiungo Wesley Sneijder halikuwemo kwenye orodha hiyo,yaan wali-mupa Xavi waka-muruka Sneijder,waka-mupa Iniesta na KUMUPA tuzo hiyo Lionel Messi.

Baada ya hapo tuzo ikawa inahama kwa mtindo wa upatu,yaan nipe nikupe kati ya Messi na Ronaldo,inatoka Madrid inaenda Madeira kusalimia,ikitoka huko inarudi tena Hispania kwenye jimbo la Katalunya na kuelekea Rosario kupiga " selfie" na washkaji,hakuna upinzani.

Siku zikapita,ikawa mchana ikawa asubuhi,majira yakasogea,Uholanzi wakapotea kwenye Ulimwengu wa soka,Sneijder akatangaza kung'atuka kwenye soka la kimataifa,akatuachia mrithi wa kazi yake,naye ni Mtakatifu machoni pa wanandinga wengi duniani,Luka Modric wa Real Madrid na timu ya taifa ya Croatia.

Luca Modric akiipigania jezi ya Croatia

Mchezaji wa nafasi ya kiungo.
Nafasi aliyokuwa anacheza Sneijder wakati yupo Madrid ndio nafasi anayocheza Modric leo hii,namba ya jezi aliyoshinda nayo UEFA Sneijder ndio namba ya jezi aliyoshinda nayo Modric na kumpa tuzo ya mchezaji bora wa dunia.

Mafanikio ya timu zao za taifa kati ya wawili hao kwenye kombe la dunia yote ni sawa,wote walishika nafasi ya pili,japokuwa Modric alimaliza na magoli mawili lakini Sneijder alimaliza na magoli matano na hakupata tuzo yoyote,FIFA walimruka....MUPE,MURUKE,MUPEE,MURUKEE,MURUKEEE........!!!!

Huko alipo najua Sneijder anafurahia tuzo ya Modric,anajihisi ni kama ameipata yeye,kwani vigezo vilivyompa tuzo Modric ndivyo hivyo hivyo vilivyomnyima Sneijder,ama kweli dunia haina usawa...!!

Luca Modric akiwa kibaruani na jezi ya Real Madrid

Kitu pekee cha kujivunia kwa Sneijder ni ile huduma ya "free delivery" ya mipira aliyokuwa anaifanya uwanjani,sasa imepata mrithi sahihi ambaye ni Luka Modric na kutambuliwa mchango wake,anakupa akitaka,anakuruka asipotaka,na anafunga kwa mateso makali kama alivyomning'iniza Willy Caballero wa Argentina kwenye kombe la dunia.

@Sir_Rwechu
©2018

HAMILTON jino kwa jino na VETTEL katika RUSSIAN GRAND PRIX

Lewis Hamilton anaongoza kwa tofauti ya alama 40 dhidi ya Sebastian Vettel 
Kuelekea mbio za Langalanga za RUSSIAN GRAND PRIX zitakazofanyika mjini SOCHI jumapili hii kampuni ya MERCEDES imesema haitabweteka licha ya dereva wake LEWIS HAMILTON kuongoza kwa alama 40 mbele ya mpinzani wake mkubwa SEBASTIAN VETTEL katika msimamo wa mbio hizo.

HAMILTON ameshinda mashindano MATATU kati ya MANNE yaliyopita na kujikusanyia jumla ya alama 281 akiwa kinara na kampuni ya FERARI chini ya dereva wake mashuhuri SEBASTIAN VERTEL anayeshika nafasi ya pili akiwa na alama 241 wana kibarua cha kupindua matokeo katika mashindano SITA yaliyosalia ambayo yana jumla ya alama 150.

Mtendaji mkuu wa MARCEDES, TOTO WOLFF anasema ni jambo jema kwao kuongoza msimamo mpaka hivi sasa na kwamba wapinzani wasifikiri kuwa watalegeza kamba na badala yake wataendelea kupambana zaidi.

Marcedes wanaimani kubwa ya kutetea taji la dunia

WOLFF anasema kampuni ya MERCEDES ilishangazwa na jinsi madereva wake walivyopambana katika mashindano SITA yaliyopita na kusisitiza kuwa sasa wanaweka umakini zaidi kwenye kila shindano lililkosalia ikiwemo kuhakikisha gari zinakuwa kwenye ubora wakati wote ili kutetea taji la dunaia.

Mbio za langalanga kwa msimu huu zimebakiza mashindano SITA tu kumalizika ambayo ni pamoja na yale yatakayofanyika nchini RUSSIA jumapili hii yakifuatiwa na yale ya JAPANI, MAREKANI, MEXICO, BRAZIL na ABU DHABI.

SINGIDA UTD Vs MBEYA CITY machozi jasho na damu NAMFUA

Singida United kuumana na Mbeya City kwenye dimba la Namfua mjini Singida
Ligi kuu Tanzania Bara inaendelea leo JUMATANO kwa kuchezwa mchezo  mmoja ambapo SINGIDA UNITED waliopo kwenye nafasi ya 14 wakiwa na alama 7 itawaalika wanakoma kumwanya, MBEYA CITY  waliopo kwenye nafasi ya 13 wakiwa na lama 7 pia mchezo utakaochezwa kwenye dimba la NAMFUA mjini SINGIDA.

Katika mchezo pekee uliochezwa jioni ya jana timu ya KMC na LIPULI FC zimeendelea na rekodi yake ya kupata sare kwenye michezo yao ya ligi kuu kwa msimu huu baada ya kutoka suluhu kwenye mchezo uliochezwa kwenye uwanja wa UHURU jijini DSM.


Katika mchezo huo uliokuwa na mashambulizi ya kushitukiza kwa pande zote mbili ulishuhudia mlinzi wa kushoto wa LIPULI FC, PAUL NGALEMA akilimwa kadi nyekundu kwenye dakika ya 90 ya mchezo huo baada ya kumchezea madhambi kiungo wa KMC, CHRIS BUYOYA.

Kwa matokeo hayo timu zote mbili zimefikisha alama SABA ambapo KMC imeshinda mchezo MMOJA na imetoka sare katika michezo MINNE na kupoteza mchezo MMOJA huku LIPULI FC wakishinda mchezo MMOJA na kutoka sare katika michezo MINNE.

LAMPARD Amshangaza MOURINHO Old Trafford

Mlinda mlango wa Derby Country akipangua mkwaju wa Phil Jones
Timu ya DERBY COUNTY inayonolewa na nyota wa zamani wa CHELSEA, FRANK LAMPARD imeitupa nje ya mashindano ya kombe la ligi MANCHESTER UNITED baada ya kuitandika kwa penati 8-7 kufuatia sare ya mabao MAWILI kwa MAWILI kwenye mchezo uliopigwa kwenye dimba la OLD TRAFFORD.

Katika mchezo huo HARRY WILSON amekuwa mchezaji wa kwanza kuifunga MANCHESTER UNITED goli la moja kwa moja la mpira wa adhabu yaani Direct Free Kick katika kombe la ligi kwenye dimba la OLD TRAFFORD tangu alipofanya hivyo GILES BARNES mwezi JANUARY mwaka 2009 wakati akifunga bao la kwanza la kusawazisha kwa DERBY COUNTRY. 

MANCHESTER UNITED imepoteza mechi zake TANO zilizopita katika mashindano yeto ambazo ziliamuliwa na changamoto ya mikwaju ya penati ambapo TATU ni za kombe la ligi, moja kwenye kombe la FA na nyingine kwenye ngao ya jamii.

Derby wamepata ushindi wa kwanza kwenye dimba la Old Trafford tangu mwaka 2001

Mlinda mlango SERGIO ROMERO ni mchezaji wa kwanza wa MANCHESTER UNITED kuoneshwa kadi nyekundu ya moja kwa moja kwenye dimba la OLD TRAFFORD katika mashindano yote tangu alipofanya hivyo mlinzi ERIC BAILLY mwezi MAY mwaka jana 2017 katika mchezo wa ligi ya YUROPA dhidi ya CELTA VIGO baada ya kuoneshwa kadi nyekundu kwenye dakika ya 67.

Wachezaji wa Derby wakishangilia moja ya goli walilowafunga Man Utd

Baadhi ya matokeo mengine ya michezo ya kombe la ligi MAN CITY wakiwa ugenini wameilaza OXFORD UNITED mabao MATATU kwa BILA, WEST BROM wamenyukwa mabao MATATU kwa BILA pia na CRYSTAL PALACE wakati BOURNAMOUTH wakiinyuka BLACKBURN ROOVERS mabao MATATU kwa MAWILI huku BURTON ALBION wakiishangaza BURNLEY kwa kuitandika mabao MAWILI kwa MOJA.

Hii leo kutakuwa na mtanange wa kukata na shoka ambapo majogoo wa jiji LIVERPOOL watakuwa nyumbani kuwakaribisha CHELSEA wakati ARSENAL wakiumana na BRENTFORD huku TOTTENHAM HOTSPURS wakiwakaribisha WATFORD.

CAF kumuunga mkono INFANTINO Urais wa FIFA

Shirikisho la soka barani Afrika CAF linamuunga mkono Infantino Rais wa shirikisho la soka barani Africa (CAF) AHMAD AHMAD amesema shir...