Jeshi
la Nigeria linasema kuwa limewaokoa zaidi ya watu 180, wengi wao
wanawake na watoto, kutoka kwa kundi hatari la wapiganaji wa kiislamu la
Boko Haram, katika jimbo la Borno.
Kupitia taarifa kwa vyombo vya
habari, msemaji moja wa jeshi amesema kuwa kambi kadhaa za waasi hao
zilizoko karibu na mji wa Maiduguri zimeharibiwa na kamanda mmoja wa
Boko Haram kukamatwa, lakini duru hizo hazijasema ni lini tukio hilo
lilifanyika.Wakati hio huo, Rais wa Niger, Mahmadou Issoufou, amesema kuwa jeshi jipya linalojumuisha wanajeshi kutoka mataifa kadhaa huko Afrika magharibi, lina uwezo mkubwa wa kukabiliana na Boko Haram.