Friday, 17 July 2015

Samsung yazindua simu nyembamba zaidi,ione hapa

null

Samsung A8
Kampuni ya Samsung imezindua simu yake nyembamba zaidi aina ya smartphone kufikia sasa.
Simu hiyo kwa jina Galaxy A8 ina upana wa milimita 5.9 ikiwa ni wembamba wa asilimia 85 ikilinganishwa na simu ya Galaxy S6 Edge.
Licha ya wembamba huo waandisi wameweza kuiweka betri pamoja na kamera yenye uwezo wa mega pikseli 16.
Samsung Galaxy A8 
 
 
 
 
 
Mmoja ya wataalam aliuliza swali la muhimu wa kutengeza simu nyembamba.
Kwa sasa Samsung imetangaza kwamba simu hiyo itauzwa nchini Uchina na Singapore.
''Galaxy A8 haitauzwa nchini Uingereza'' alisema msemaji wake.
Ijapokuwa itakuwa simu nyembamba zaidi kutoka kwa mojwapo ya kampuni kubwa ,kampuni nyengine za Uchina tayari zimeanza kuuza simu kama hizo.

Ibada ya Eid yakumbwa na gundu huko Nigeria,watu wafa kama kuku leo



Mlipuko

Jeshi nchini Nigeria linasema kuwa takriban watu 11 wameuawa kwenye mashambulizi mawili ya kujitoa mhanga kwenye mji ulio kaskazini mashariki mwa nchi wa Damaturu.
Wanasema kuwa washambuliaji wote walikuwa ni wanawake , mmoja mwenye mri mkubwa na mwingine mwenye umri wa miaka kumi.
Ripoti zingine zinasema kuwa idadi ya waliokufa ni kubwa.
Mashambulizi mengine yalifanyika kwenye maombi ya kusherehekea siku kuu ya Eid ul Fitr ya kumaliza mwezi mtukufu wa Ramadhan.
Mashambulizi kama hayo hulaumiwa kwa kundi la kiislamu la Boko Haram ambalo limeongeza mashambulizi yake tangu rais Muhammadu Buhari aingie madarakani.

CAF kumuunga mkono INFANTINO Urais wa FIFA

Shirikisho la soka barani Afrika CAF linamuunga mkono Infantino Rais wa shirikisho la soka barani Africa (CAF) AHMAD AHMAD amesema shir...