Friday, 17 July 2015

Ibada ya Eid yakumbwa na gundu huko Nigeria,watu wafa kama kuku leo



Mlipuko

Jeshi nchini Nigeria linasema kuwa takriban watu 11 wameuawa kwenye mashambulizi mawili ya kujitoa mhanga kwenye mji ulio kaskazini mashariki mwa nchi wa Damaturu.
Wanasema kuwa washambuliaji wote walikuwa ni wanawake , mmoja mwenye mri mkubwa na mwingine mwenye umri wa miaka kumi.
Ripoti zingine zinasema kuwa idadi ya waliokufa ni kubwa.
Mashambulizi mengine yalifanyika kwenye maombi ya kusherehekea siku kuu ya Eid ul Fitr ya kumaliza mwezi mtukufu wa Ramadhan.
Mashambulizi kama hayo hulaumiwa kwa kundi la kiislamu la Boko Haram ambalo limeongeza mashambulizi yake tangu rais Muhammadu Buhari aingie madarakani.

No comments:

Post a Comment

CAF kumuunga mkono INFANTINO Urais wa FIFA

Shirikisho la soka barani Afrika CAF linamuunga mkono Infantino Rais wa shirikisho la soka barani Africa (CAF) AHMAD AHMAD amesema shir...