Thursday, 3 March 2016

tazama : Waasi wa LRA, waendelea kuteka watoto.


Image copyright Reuters
Image caption Joseph Kony
Kundi la waasi la LRA limewateka nyara watu 217 katika Jamhuri ya Afrika ya kati, toka kuanza kwa mwaka huu.
Shirika la Invisible Chldren limesema kati ya hao, watoto ni 54 ambao wanatumika kama askari, wafanyakazi ndani ya kambi zao na wale wanaotumiwa kingono.
Utekaji nyara huo unaelezwa pia ni kama jaribio la kutaka kujazia jeshi lake.
Kundi hilo limekuwa likihangaika kujipanga upya, tangu majeshi ya kigeni yalipoanza mashabulizi dhidi yake mwaka 2011.
Marekani ilipeleka kikosi maalumu cha wanajeshi 100 mwaka 2011, kuunga mkono maelfu ya wanajeshi wa Afrika wanaowasaka makamanda wake, akiwemo kiongozi wao Joseph Kony.

Mwandishi ''wa al-Shabab'' ahukumiwa kifo


























Image copyright n
Image caption Wapiganaji wa al-shabab

Mahakama ya kijeshi katika mji mkuu wa Somalia,Mogadishu imempatia hukumu ya kifo mwandishi anayedaiwa kupanga njama ya mauaji ya waandishi wengine nchini humo.
Hassan Hanafi,ambaye ni mwanachama wa kundi la kigaidi la al-Shabab alikamatwa nchini Kenya mnamo mwezi Agosti akitoroka.
Mahakama iliamuru kwamba anafaa kuuawa kwa kupigwa risasi.
Upande wa Mashtaka ulimshtumu kwa kuwaua waandishi wengine maarufu nchini Somalia mwaka 2007.
Hanafi alijiunga na wapiganaji wa kundi la al-Shabab miaka michache iliopita baada ya kufanya kazi na Redio Andalus,ambayo ndio inayotoa taarifa za kundi hilo.
Kukingana na kamati inayowalinda waandishi katika shirika la waandishi duniani,waandishi 59 wameuawa nchini Somalia tangu mwaka 1992 na 33 tangu mwaka 2007.

VIDEO: TAZAMA NA DOWNLOAD WIMBO MPYA WA HARMONIZE FT DIAMOND PLATNUMZ - BADO HAPA

CAF kumuunga mkono INFANTINO Urais wa FIFA

Shirikisho la soka barani Afrika CAF linamuunga mkono Infantino Rais wa shirikisho la soka barani Africa (CAF) AHMAD AHMAD amesema shir...