Thursday, 4 June 2015

tazama picha za matukio ya xavi na picha zake akiagwa barcelona .alia kwa uchungu.


XAVI4
 Kuelekea fainali ya Ligi ya Mabingwa kati ya Barcelona dhidi ya Juventus, kiungo Xavi mwenye umri wa miaka 35 alipewa heshima katika klabu ambayo aliitumikia kwa muda mrefu tangu ana umri wa miaka 11 alipojiunga nayo.
XAVI
Fainali hiyo inayosubiriwa na watu wengi itafanyika siku ya Jumamosi.
Xavi ameshindwa kuzuia hisia zake na kumwaga machozi wakati wa shamrashamra za kumuaga ndani ya klabu yake ya Barcelona kuelekea fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Juventus.
XAVI2
Xavi amemshukuru kocha Luis Enrique kwa kumuwezesha kubaki katika klabu hiyo msimu uliopita huku akishindwa kuvumilia maneno ya Iniesta aliposimama na kumuaga kwa niaba ya wachezaji wenzake.
XAVI3
Kiungo huyo alitangaza mwezi uliopita kwamba anakwenda kumalizia soka yake katika klabu ya Al-Sadd ya Qatar mwishoni mwa msimu, akihitimisha miaka yake 24 kuwa na vigogo hao.
XAVI6

mrembo matata afariki dunia akiwa anaongeza makalio huko marekeni. soma hii ni muhimu sana kwa wanawake wote.

 Alitamani kuwa na makalio makubwa, baada ya kuchomwa sindano matokeo ilikuwa ni stori nyingine !!
Syringe
Ishu ya wasichana na wanawake kupenda kuongeza maumbile ya miili yao limekua kama ishu ambayo imechukua sana nafasi sehemu mbalimbali duniani.
Tunashuhudia watu wengi wakiongeza makalio kwa kusudi la kuwa wenye mvuto zaidi, na kumekuwepo na vidonge na sasa kuna sindano za kuongeza makalio.
Mahyew
Kelly Mayhew
Leo nimekutana na stori iliyotokea Los Angeles Marekani, ambako msichana Kelly Mayhew mwenye miaka 34 amefariki baada ya kufikishwa St.John’s Espiscopal Hospital, muda mfupi baada ya kuchomwa sindano ya kuongeza makalio.






Kelly Mayhew  Photo via Facebook



Kelly Mayhew  Photo via Facebook
Kelly Mayhew na mama yake walisafiri kutoka Maryland kwenda Rockaway, walikokua wameelekezwa na rafiki yake Kelly ili kwenda kuchoma sindano hiyo ambayo ilikua inatolewa kinyume na utaratibu… mtoaji wa huduma hiyo alijiita daktari lakini hakuwa amesajiliwa na alikuwa hatambuliki kisheria.
Baada ya kuchomwa sindano hiyo, Kelly alianza kupumua kwa shida, akawa anajitupa ovyo chini huku akiishiwa pumzi… baada ya kuhangaika kwa kama dakika ishirini hivi, Kelly alifariki akiwa kwenye mikono ya mama yake.. mpaka Polisi wanafika eneo hilo Daktari alikuwa tayari kashakimbia.



KAULI YA MWISHO YA KOFI ANNAN KWA NKURUNZINZA HII HAPA















Aliyekuwa katibu mkuu wa umoja wa mataifa Koffi Annan amemtaka rais wa Burundi Pierre Nkurunziza kujiuzulu huku uchaguzi mkuu ukiahirishwa.
Kumekuwa na maandamano ya ghasia nchini Burundi pamoja na mapinduzi yaliofeli tangu Nkurunziza atangaze kuwa atawania muhula mwengine wa tatu wa urais katika kile watu wanaamni ni ukiukaji wa katiba.
Annan ameiambia BBC kwamba rais huyo amepoteza uhalali wake na sasa anafaa kujiuzulu iwapo anawajali raia wa Burundi.

Matamshi hayo ya Annan yataongeza shinikizo kwa rais Nkurunziza ,ambaye hadi sasa hajatoa ishara zozote za kujiuzulu.
Uchaguzi wa bunge pamoja na ule wa urais umehairishwa kufuatia wiki za maandamano ya ghasia.
Viongozi wa jumuia ya Afrika Mashariki walipendekeza uchaguzi wa bunge na urais uahirishwe kwa wiki sita kufuatia ghasia za kumpinga rais Pierre Nkurunziza kuwania muhula wa tatu.
Rais wa Burundi Pierre Nkurun












CAF kumuunga mkono INFANTINO Urais wa FIFA

Shirikisho la soka barani Afrika CAF linamuunga mkono Infantino Rais wa shirikisho la soka barani Africa (CAF) AHMAD AHMAD amesema shir...