Aliyekuwa katibu mkuu wa umoja wa
mataifa Koffi Annan amemtaka rais wa Burundi Pierre Nkurunziza kujiuzulu
huku uchaguzi mkuu ukiahirishwa.
Kumekuwa na maandamano ya ghasia
nchini Burundi pamoja na mapinduzi yaliofeli tangu Nkurunziza atangaze
kuwa atawania muhula mwengine wa tatu wa urais katika kile watu wanaamni
ni ukiukaji wa katiba.Annan ameiambia BBC kwamba rais huyo amepoteza uhalali wake na sasa anafaa kujiuzulu iwapo anawajali raia wa Burundi.
Matamshi hayo ya Annan yataongeza shinikizo kwa rais Nkurunziza ,ambaye hadi sasa hajatoa ishara zozote za kujiuzulu.
Uchaguzi wa bunge pamoja na ule wa urais umehairishwa kufuatia wiki za maandamano ya ghasia.
Viongozi wa jumuia ya Afrika Mashariki walipendekeza uchaguzi wa bunge na urais uahirishwe kwa wiki sita kufuatia ghasia za kumpinga rais Pierre Nkurunziza kuwania muhula wa tatu.
No comments:
Post a Comment