![]() |
Wachezaji wa Yanga katika moja ya mazoezi yao |
Taarifa mbalimbali zinasema kuwa uongozi wa klabu ya Yanga ya jiji DSM umewasamehe wachezaji wake watatu viungo Said Makapu na Pius Buswita pamoja na beki wa kushoto Haji Mwinyi ambao hawakuwa sehemu ya mchezo uliopita dhidi ya Stand United kwa kile kilichoelezwa kuwa ni utovu wa nidhamu.
Wachezaji hao waliondolewa kambini na Kocha Mkuu wa Yanga, Mkongomani Mwinyi Zahera kwa utovu wa nidhamu na sasa watakuwa sehemu ya kikosi kuelekea mechi zijazo za Ligi Kuu Bara ikiwemo ya mwishoni mwa juma dhidi ya Singida United.
![]() |
Kocha wa Yanga Mwinyi Zahera |
Imeelezwa kuwa wachezaji hao wameomba radhi kwa Kocha wao ambaye ameonekana kuwa mbogo kwa wale wote wanaoleta ujuaji ndani ya timu bila sababu za msingi.