Friday, 21 September 2018

NAOMI OSAKA AZIDI KUWAPA TABU

Naomi Osaka Bingwa wa US OPEN 
Kinda wa Japan Naomi Osaka atamenyana na Barbara Strycova wa jamhuri ya Czech katika mchezo wa robo fainali ya mashindano ya wazi ya Pan Pacific yanayofanyika jijin Tokyo.

Nyota huyo anayeshika nafasi ya TATU kwenye viwango vya ubora ametinga hatua ya robo fainali baada ya kumtandika bila ya huruma Dominika Cibulkova seti mbili kwa bila za ushindi wa 6-2 6-1 ukiwa ni mchezo wake wa kwanza tangu ashinde taji la mashindano ya wazi ya marekani.

NAOMI mwenye miaka 20 bado anakumbukwa baada ya kumnyuka mkongwe Serena Williams na kushinda taji lake la kwanza la mashindano makubwa (GRANDSLUM) mapema mwezi huu katika fainali ambayo SERENA alizozana vikali na mwamuzi wa mchezo huo.

No comments:

Post a Comment

CAF kumuunga mkono INFANTINO Urais wa FIFA

Shirikisho la soka barani Afrika CAF linamuunga mkono Infantino Rais wa shirikisho la soka barani Africa (CAF) AHMAD AHMAD amesema shir...