Tuesday, 14 July 2015

kombe la kagame hili hapa tena katika viwanja vya tanzania


Rais wa Rwanda Paul Kagame
Michuano ya klabu bingwa Afrika Mashariki na Kati jumamosi wiki hii inaanza kutimua vumbi mjini Dar es Salaam Tanzania huku jumla ya vilabu 13 vikishiriki.
Rais wa Rwanda Paul Kagame anatarajiwa kutoa kiasi cha dola elfu 60 za marekani kama zawadi kwa washindi.
Kundi A itajumuisha timu za Yanga yaTanzania, Gor Mahia ya Kenya, Kmkm Zanzibar, Telecom ya Djibout na Khartoum- Sudani Kaskazini.
Kundi B - APR Rwanda, Al Shandy ya Sudan, LLB FC Burundi naHeegan Somalia.
Wakati kundi C - Azam ya Tanzania, Malakia ya Sudan Kusini, Adama ya Ethiopia na KCCA ya Uganda.
Hata hivyo mgawanyo wa zawadi kwa kila mshindi ni kwamba mshindi wa kwanza atajinyakulia dola elfu 30, wa pili dola elfu 20 na wa tatu dola elfu 10.

EBOLA YARUDI TENA KWA KASI AFRIKA YA MAGHARIBI.

null

Wataalam wa afya dhidi ya Ebola
Maofisa wa afya nchini Sierra Leone wametahadharisha uwezekano wa kutokea maambukizi zaidi ya virusi vya ugonjwa wa Ebola ikiwa ni mwaka mmoja tangu mgonjwa wa kwanza kubainika nchini humo. Wamesema kuwa hofu ya baadhi ya watu kukataliwa na kutengwa na jamii ni moja ya sababu inayochangia kuenea kwa maambukizi hayo kwani wengi hujificha wanapokumbwa na ugonjwa huo. Hata hivyo kumekuwa na kasi ya kupungua kwa maambukizi ya ugonjwa huo katika siku za hivi karibuni ,japo kuwa katika makao makuu ya nchi hiyo Freetown hivi karibuni kumekuwa na maambukizi mapya ya ugonjwa huo. Zaidi ya watu 4000 walikufa kutokana na ugonjwa wa Ebola nchini Liberia na hivyo kuifanya nchi hiyo kuwa moja ya nchi tatu zilizoathirika na Ebola,zikiwemo Guinea na Liberia.

CAF kumuunga mkono INFANTINO Urais wa FIFA

Shirikisho la soka barani Afrika CAF linamuunga mkono Infantino Rais wa shirikisho la soka barani Africa (CAF) AHMAD AHMAD amesema shir...