Tuesday, 16 February 2016

valentine`s day Mbunge Zimbabwe avunja rekodi ya kulana mate na mkewe Afrika.



Image captionMbunge Joseph Chinotimba Zimbabwe
Mbunge mmoja nchini Zimbabwe Joseph Chinotimba ameingia katika kumbukumbu za Afrika baada ya kumbusu mke wake Vimbai kwa muda mrefu zaidi kuwahi kunakiliwa barani Afrika.
Mbunge huyo na mkewe walizoa tuzo hilo baada ya kupigana busu kwa dakika 10 na sekunde 17.
Rekodi hiyo iliwekwa katika hafla moja iliyopigiwa upatu na kunadiwa kuwa ''Mashindano ya busu refu zaidi kuwahi barani Afrika''
Image captionBwana Chinotimba na mkewe Vimbai
Hafla hiyo ilipangwa na kuandaliwa kwa ushirikiano na waandalizi wa Daftari la rekodi barani Afrika.
Hafla hiyo iliandaliwa katika mji mkuu wa Harare kama sehemu ya kuadhimisha sikukuu ya wapendanao iliyoadhimishwa jumapili.

Al-Shabab wavamia kambi ya jeshi Somalia, tazama picha za tukio hapa


Image captionWapiganaji wa al-shabab
Wapiganaji wa kundi la kigaidi la al-Shabab wamevamia vituo vya polisi pamoja na kambi ya wanajeshi karibu na mji mkuu wa Somalia Mogadishu.
Mji wa Afgoye ulionekana kuwa eneo salama, japo wapiganaji hao walivamia nyakati za usiku na kuua watu kumi, wengi wao wakiwa wanajeshi wa asili ya kisomali.
Wapiganaji hao wa al Shabab walichukua silaha kali na magari ya kijeshi.
Wanajeshi wa Umoja wa Afrika wanasaidi wanajeshi wa Somalia kulinda taifa hilo, japo mashambulizi ya hivi karibuni yamedhoofisha usalama nchini humo.

CAF kumuunga mkono INFANTINO Urais wa FIFA

Shirikisho la soka barani Afrika CAF linamuunga mkono Infantino Rais wa shirikisho la soka barani Africa (CAF) AHMAD AHMAD amesema shir...