Tuesday, 5 May 2015

maelfu ya watu wakimbia nchini nigeria kuhofia kuuwawa na boko haram.tazama waafrika wenzetu wanavyoteseka


Watu wapatao elfu tano wamevikimbia visiwa katika Ziwa Chad kusini-mashariki mwa Niger wakihofia mashambulizi mapya ya kundi la kigaidi la Boko Haram ambalo linaandamwa vikali nyumbani nchini Nigeria.
Wakaazi wa visiwa vya Ziwa Chad wakijiandaa kuondoka
Wakaazi wa visiwa vya Ziwa Chad wakijiandaa kuondoka
Afisa wa Umoja wa Mataifa ameliambia shirika la habari la Ufaransa-AFP, kuwa zaidi ya watu 5,000 tayari wamewasili N'Guigmi, mji ulioko kusini-mashariki mwa Niger unaopakana na Chad. Amesema wengine 11,500 wanatarajiwa kuwasili kwenye mji huo. Wiki iliyopita maafisa wa Niger, waliwataka wakaazi wa maeneo ya karibu na Ziwa Chad kuondoka kwenye visiwa hivyo ifikapo jana Jumatatu, ikihofia uwezekano wa Boko Haram kushambulia visiwa hivyo.
Moussa Tchangari, mkuu wa shirila la Niger lisilo la kiserikali, amesema maelfu ya wanaume, wanawake, watoto na wazee, walitembea umbali wa kilomita 50 hadi kuufikia mji wa N'Guigmi. Tchangari amesema watu hao walikuwa wamechoka kupita kiasi, wana njaa na kiu, wakati walipowasili mjini humo.
Hata hivyo, amesema mji huo haukuwa umeandaliwa kwa ajili ya kuwapokea na kuwasaidia maelfu ya watu hao,
Mmoja wa wanawake waliookolewa
Mmoja wa wanawake waliookolewa
shutuma ambazo zimekanushwa na maafisa wa serikali ya Niger. Gavana wa Diffa, amesema leo kuwa kila kitu kinakwenda vizuri. Duru za Umoja wa Mataifa, zimeeleza kuwa serikali imeanza kugawa misaada.
Wakati huo huo Kundi la kigaidi la Boko Haram liko katika hatari ya kuvunjika baada ya mvutano kuzuka kati ya wapiganaji na viongozi wa kundi hilo. Inadaiwa kuwa mvutano huo unachochewa na uhaba wa silaha. Mvutano huo unazuka wakati ambapo majeshi ya serikali yanazidi kusonga mbele.
Wanawake waliookolewa waelezea hali halisi
Taarifa hizo ni kwa mujibu wa wanawake waliookolewa na serikali kutoka kwa wapiganaji hao wa jihadi, waliokuwa wanashikiliwa mateka tangu mwaka jana. Wamesema wapiganaji wa Boko Haram walikuwa wakiwalalamikia kutokana na uhaba wa bunduki, risasi na mabomu, huku baadhi yao wakitumia fimbo na baadhi ya magari kuharibika au kukosa mafuta na kwamba vikosi vya serikali vinakaribia kulifikia eneo waliko la Sambisa.
Mmoja wa wanawake hao, Salamatu Mohamed amesema siku waliookolewa na wanajeshi wa serikali, wanamgambo hao waligundua kuna helikopta mbili za jeshi zikizunguka kwenye eneo hilo. Anasema baada ya kuona hivyo, wapiganaji hao wakaanza kuwauza kwa Dola 10 kila mmoja. Hata hivyo anasema baadhi ya wanawake walikataa na kuanza kukimbia baada ya kuanza kupigwa kwa mawe.
Wanajeshi wa Nigeria wanaopambana na Boko Haram
Wanajeshi wa Nigeria wanaopambana na Boko Haram
Msemaji wa shirika la kitaifa la usimamizi wa masuala ya dharura-NEMA katika jimbo la Adamawa, Sa'adou Bello, amesema wanawake 700 pamoja na watoto waliookolewa hivi karibuni wataanza kupatiwa matibabu na wengi wao wanaonyesha dalili za kupatwa na kiwewe.
''Hatutawapeleka moja kwa moja kwenye familia zao, hadi tuwafanyie uchunguzi wa kitaalamu na mtu yeyote atakayekutwa na matatizo atapatiwa matibabu kabla ya kurudishwa,­'' alisema Bello.
Katika miezi ya hivi karibuni jeshi la Nigeria kwa kushirkiana na majeshi ya nchi jirani ya Chad, Cameroon na Niger, yaliripoti kulishinda kundi la Boko Haram baada ya kuwafurumusha kwenye maeneo mengi waliyokuwa wanayadhibiti.

van perse kuanzia sasa hana tena nafasi ya kupiga penalti katka kipindi chote atakachokua anaichezea manchester united



Louis Van Gaal

Mkufunzi wa kilabu ya Manchester United Louis Van Gaal amempokonya mshambuliaji wa kilabu hiyo Robin Van Persie haki za kupiga mkwaju wa penalti baada ya kukosa mkwaju kama huo katika mechi dhidi West Brom.
Alipoulizwa iwapo Van Persie angeendelea kama mchezaji aliyeorodheshwa kupiga penalti kwa niaba ya kilabu hiyo alijibu ''hapana,amefika mwisho wake.Kila mara anarejelea makosa hayo hayo aliongezea''.
''Wayne Rooney pia amekosa mkwaju wa penalti na unapokosa mkwaju huo basi ujue utapiga foleni''.,aliongezea

Van Persie

Ushindi wa West Brom ulikuwa matokeo mabaya kwa upande wa Manachester United kwa mara ya tatu mfululizo.
Van Persie mwenye umri wa miaka 31 alikuwa na fursa ya kusawazisha kufuatia bao la Chris Brunty kunako dakika ya 63 baada ya refa Anthony Taylor kumpata na Saido Berahino na makosa ya kuunawa mpira katika eneo la hatari.

CAF kumuunga mkono INFANTINO Urais wa FIFA

Shirikisho la soka barani Afrika CAF linamuunga mkono Infantino Rais wa shirikisho la soka barani Africa (CAF) AHMAD AHMAD amesema shir...