Tuesday, 5 May 2015

van perse kuanzia sasa hana tena nafasi ya kupiga penalti katka kipindi chote atakachokua anaichezea manchester united



Louis Van Gaal

Mkufunzi wa kilabu ya Manchester United Louis Van Gaal amempokonya mshambuliaji wa kilabu hiyo Robin Van Persie haki za kupiga mkwaju wa penalti baada ya kukosa mkwaju kama huo katika mechi dhidi West Brom.
Alipoulizwa iwapo Van Persie angeendelea kama mchezaji aliyeorodheshwa kupiga penalti kwa niaba ya kilabu hiyo alijibu ''hapana,amefika mwisho wake.Kila mara anarejelea makosa hayo hayo aliongezea''.
''Wayne Rooney pia amekosa mkwaju wa penalti na unapokosa mkwaju huo basi ujue utapiga foleni''.,aliongezea

Van Persie

Ushindi wa West Brom ulikuwa matokeo mabaya kwa upande wa Manachester United kwa mara ya tatu mfululizo.
Van Persie mwenye umri wa miaka 31 alikuwa na fursa ya kusawazisha kufuatia bao la Chris Brunty kunako dakika ya 63 baada ya refa Anthony Taylor kumpata na Saido Berahino na makosa ya kuunawa mpira katika eneo la hatari.

No comments:

Post a Comment

CAF kumuunga mkono INFANTINO Urais wa FIFA

Shirikisho la soka barani Afrika CAF linamuunga mkono Infantino Rais wa shirikisho la soka barani Africa (CAF) AHMAD AHMAD amesema shir...