Wednesday, 18 May 2016

Soma hii: Wapiganaji wa Kiislamu wadai 'wamo Tanzania'



ISImage copyrightREUTERS
Image captionAliyesambaza video hiyo anasema wana uhusiano na Islamic State
Kundi la watu wanaojidai kuwa wapiganaji wa Kiislamu limeweka video mtandaoni likidai uwepo wa wa wapiganaji wa Kiislamu nchini humo.
Video hiyo inawaonesha wanaume hao wakiwa wamejifunika nyuso zao kwa vitambaa na barakoa.
Wanadai wamo katika mji wa Tanga na kuwahimiza Waislamu katika taifa hilo la Afrika Mashariki kujiunga na kampeni yao.
Ukurasa wa Twitter ambao unasambaza video hiyo ya dakika tano unasema wanaume hao ni tawi la Afrika Mashariki la kundi linalojiita Islamic State (IS).
Mwandishi wa BBC anayeangazia masuala ya usalama Afrika, Tomi Oladipo, anasema hakuna ushahidi wa uhusiano wa moja kwa moja kati ya wapiganaji hao na kundi la Islamic State.
Serikali ya Tanzania imesema inafahamu uwepo wa video hiyo pamoja na ujumbe uliochapishwa kwenye Twitter na inafanya uchunguzi kubaini uhalisi wake.
Waziri wa mambo ya ndani Charles Kitwanga ameambia BBC kwa njia ya simu kwamba serikali inachukulia habari hizo kwa uzito akisema zinaweza kutishia usalama wa taifa.

Unyama: tazama video, mwanamke amkata mumewe sehemu nyeti.

HIVI PUNDE: Ndege ya Misri yapotea ikitoka Paris


  • Saa moja iliyopita
NdegeImage copyrightAFP
Image captionMwezi Machi ndege nyingine ililazimishwa kuelekea Cyprus
Ndege moja ya shirika la ndege la Misri la EgyptAir, iliyokuwa ikitoka mji mkuu wa Ufaransa Paris hadi Cairo, imetoweka kutoka kwenye mitambo ya rada.
Maafisa wanaosimamia safari za ndege wanasema kuwa ndege hiyo aina ya Airbus A320, ilikuwa na abiria 59 na wahudumu kumi.
Shirika hilo limesema kuwa ndege hiyo ilitoweka katika maeneo ya mashariki ya bahari ya Mediterranean, kilomita 16 kabla ya kufika katika anga ya Misri.
Hakuna dalili zozote za kuwepo kwa hali mbaya ya anga.
Misri imetuma ndege za kivita kusaka ndege hiyo kwa ushirikiano na utawala wa Ugiriki.

CAF kumuunga mkono INFANTINO Urais wa FIFA

Shirikisho la soka barani Afrika CAF linamuunga mkono Infantino Rais wa shirikisho la soka barani Africa (CAF) AHMAD AHMAD amesema shir...