Saturday, 21 May 2016

Video 10 kali kwa East Africa zilizotajwa na kituo cha TV cha Sound City cha Nigeria, watanzania 6


Jumamosi ya May 21 2016 stori ambayo imegonga headlines za muziki wa Bongo fleva ni kutoka Nigeria katika kituo cha TV cha Sound City, kituo ambacho ni moja kati ya vituo vinavyocheza video zenye viwango vya kimataifa, Sound City weekend hii imecheza TOP 10 ya video kali East Africa, kwa upande wa Tanzania wasanii sita walifanikiwa video zao kuwa katika list hiyo.View image on Twitte


10- Ben Pol – Moyo Mashine

9- Nedy Music ft Ommy Dimpoz ‘Usiende Mbali’

8- Navio – Njogereza

7- Jaguar ft Mafikizolo ‘Going Nowhere’

6- Alikiba ‘Lupela’

5- Sauti Sol ‘Unconditional Bae’

4- Vanessa Mdee ‘Niroge’

3- Kayumba ‘Katoto’

2- Eddy Kenzo ft Niniola – Mbilo Mbilo
1- G Nako ‘Original

U

video: tazama waziri Kitwanga akijibu swali akiwa amelewa bungeni na kusimamishwa kazi.

Maporomoko ya ardhi yawaua zaidi ya watu 70 na wengine 120 hawajulikani walipo.



Image captionMafuriko nchini Sri Lanka.
Utawala nchini Sri Lanka unasema kuwa zaidi ya watu 70 sasa wanafahamika kuaga dunia kwenye maporomoko ya udongo yaliyosababishwa na mvua kubwa.
Zaidi ya watu wengine 120 bado hawajulikani waliko.
Katika maeneo mengine ya mji mkuu Colombo, maji yalipungua kwa kiasi leo Jumamosi lakini kwenye sehemu zingine maelfu ya watu waliolazimika kuhama kutokna na mafuriko na maporomoko ya Udongo bado wanaishi kwenye makao ya muda.
Misaada ya dharura yakiwemo mahema na mashua sasa vinawazili kutoka nchini India.

Mtu apigwa risasi kwa kubeba bunduki nje ya Ikulu


  • 21 Mei 2016
Image copyrightAP
Image captionIkulu ya White House
Afisa wa usalama wa Marekani amempiga risasi na kumjeruhi mwanamume mmoja aliyeonekana amebeba bunduki nje ya Ikulu ya White House.
Maafisa wa Usalama wamesema kuwa mtu huyo alielekea kwenye mojawapo wa milango ya kuingia katika Ikulu huku amebeba silaha hiyo. Alipoamriwa aiweke chini silaha hiyo chini akakaidi.
Image copyrightAP
Image captionWalinzi kwenye Ikulu ya White House
Watu walizuiliwa kukaribia Ikulu hiyo ya White House kwa muda, huku maafisa wa Usalama wakikimbia kuhakikisha kuwa Makamu wa Rais Joe Biden, aliyekuwa katika jengo hilo wakati huo, alikuwa salama.
Rais Obama alikuwa ameondoka kwenda kucheza mpira wa gofu.
Walioshuhudia tukio hilo walisema kuwa walisikia mlio wa risasi na kisha wakamwona mwanamume mmoja mzungu akianguka chini.

waziri afutwa kazi na rais kwa kuwa mlevi, mtazame hapa.


Image captionYaripotiwa kuwa bwana Kitwanga alienda bungeni na kujibu swali la mbunge akiwa mlevi.
Waziri wa mambo ya ndani nchini Tznania Charles Kitwanga amefutwakazi kutokana na sababu ya kuwa mlevi akiwa kazini.
Kwenye taarifa, rais John Magufuli alisema kuwa bwana Kitwanga alienda bungeni na kujibu swali la mbunge akiwa mlevi.
Hata hivyo bwana Kitwanga hajasema lolote.
Image copyrightSTATEHOUSE TANZANIA
Image captionRais John Magufuli
Rais Magufuli ambaye aliingia ofisini mwaka uliopita aliahidi kupambana na ufisadi na awewafuta kazi maafisa kadha kuhusiana na suala la ufisadi.
Lakini waandishi wa habari wanasema kuwa kufutwa kwa bwana Kitwanga ni jambo la kushangaza kwa sababu amekuwa rafiki wa rais kwa siku nyingi.

CAF kumuunga mkono INFANTINO Urais wa FIFA

Shirikisho la soka barani Afrika CAF linamuunga mkono Infantino Rais wa shirikisho la soka barani Africa (CAF) AHMAD AHMAD amesema shir...