Tuesday, 17 May 2016

Simanzi: Wana kijiji 5 wafariki wakitafuta maji .


Image copyrightAP
Image captionUkame nchini India wasababisha uhaba wa maji
Wana kijiji watano katika eneo lililokumbwa na ukame kaskazini mwa India wamefariki wakijaribu kutafuta maji katika kisima kisichotumika.
Wanaume hao walifariki baada ya kuvuta gesi ilio na hewa chafu ambayo ilikuwa ndani ya kisima hicho katika jimbo la Haryana kulingana na afisa mmoja.
Eneo kubwa la India linakabiliwa na ukame mbaya ambao umewaua takriban watu 300.
Haryana na majimbo mengine wiki iliopita yalikosolewa na mahakama ya juu nchini India kwa kushindwa kutambua tatizo hilo la maji.
Image copyrightAFP
Image captionUhaba wa maji India
Ripoti katika eneo hilo zinasema kuwa wanaume hao kutoka wilaya ya Jindi huko Haryana waliamua kujaribu kukitengeza kisima hicho ili kuweza kukabiliana na ukosefu wa maji katika eneo hilo.
Lakini naibu afisa wa polisi katika wilya hiyo Virender Singh alikana kwamba walihitaji maji ya kunywa akisema wanaume hao walitaka kukitumia kisima hicho kwa maji ya kuoga na kuosha.
''Kisima hicho kilikuwa hakijatumika kwa takriban miaka mitano hadi sita na gesi yenye sumu ilikuwa imetanda huko chini'',aliambia kituo cha habari cha AFP.

Tazama huu ‘ukatili’ wa polisi kwa wananchi kenya,mashirika yaingilia kati.



PolisiImage copyrightREUTERS
Image captionPolisi walitumia marungu kuwakabili baadhi ya waandamanaji
Mashirika ya kutetea haki za kibinadamu nchini Kenya yameshutumu maafisa wa polisi wakisema walitumia nguvu kupita kiasi kukabili waandamanaji jijini Nairobi Jumatatu.
Tume ya Taifa ya Haki za Kibinadamu (KNHRC) imesema imeshangaza sana na video na picha ambazo zinaenea kwenye mitandao ya kijamii na vyombo vya habari kuhusu yaliyojiri wakati wa maandamano hayo.
Picha hizo zinawaonesha polisi wakiwakabili waandamanaji kwa marungu.
Baadhi ya wakenya mtandaoni pia wamekuwa wakiwashutumu maafisa wa polisi na kitambulisha mada #StopPoliceBrutality (Komesha Ukatili wa Polisi) kinavuma Kenya.
Kwa mujibu wa kituo cha redio cha Capital FM jijini Nairobi, mmoja wa waliokabiliwa na polisi alifariki baadaye akipokea matibabu.
"Kikosi cha Polisi ni kikosi cha nidhamu na si kikosi cha kutumia nguvu. Kanuni ziko wazi kuhusu jinsi ya kuwashughulikia raia wakati wa maandamanaji,” tume hiyo imesema kupitia Twitter.
Mamlaka huru ya kiraia inayofuatilia shughuli za polisi (IPOA) pia imeshutumu vitendo vya maafisa wa polisi na kusema walivuka mipaka.
Mwenyekiti wa mamlaka hiyo Bw Macharia Njeru amewaambia wanahabari kwamba polisi walitumia nguvu kupita kiasi.
Amesema maafisa wa mamlaka hiyo wanakamilisha uchunguzi na watawasilisha ripoti kwa Mkurugenzi wa Mashtaka ya Umma (DPP) ili hatua zichukuliwe dhidi ya maafisa husika.
Image copyrightAP
Muungano wa upinzani CORD umekuwa ukifanya maandamano Jumatatu kila wiki kuwashinikiza maafisa wakuu wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (IEBC) wajiuzulu.
Viongozi wa CORD wamesema maafisa hao hawawezi kusimamia uchaguzi huru na wa haki wakati wa uchaguzi mkuu ujao 2017.
Wameahidi kuendelea na maandamano hayo hadi maafisa hao watakapong’atuka.

CAF kumuunga mkono INFANTINO Urais wa FIFA

Shirikisho la soka barani Afrika CAF linamuunga mkono Infantino Rais wa shirikisho la soka barani Africa (CAF) AHMAD AHMAD amesema shir...