
Tuesday, 11 August 2015
TAZAMA HII KALI....Ng'ombe 'waandamana' kupinga bei duni ya Maziwa ..
Ushawahi kukutana na ngo'mbe katika maduka ya jumla?
Na ushawahi kusikia maandamano yanayojumuisha ng'ombe ?
Amini usiamini wanunuzi katika maduka ya kifahari katika mji ya Asda Queensway, Stafford Uingereza walipigwa na butwaa ng'ombe walipoingia dukani humo !
Yamkini mifugo hao waliletwa humo na wakulima waliokuwa wakiandamana kupinga bei duni ya maziwa wanaoyolipwa na uongozi wa maduka hayo ya jumla.
Wakulima 70 wakiandamana na ng'ombe wawili walishiriki katika maandamano hayo ya kipekee.
Mnunuzi mmoja Adam Williams aliiambia BBC kuwa hata wahudumu wa duka hilo hawakuficha mshangao uliowakumba.
Walipigwa na butwaa wote ng'ombe walipoingia dukani!''
Walisababisha hali ya mshikemshike kwani walifululiza hadi upande wa ndani kabisa ya duka hilo!''
Wakulima hao wanataka maduka hayo ya jumla yawaongezee bei ya maziwa ili na wao waweze kujikimu kimaisha.
Hata hivyo wasimamizi wa maduka hayo ya jumla wanasema kuwa hilo halitafanyika.
Wanadai kuwa hakuna uhusiano wowote wa bei ya juu ya maziwa katika maduka yao na bei duni wanayolipwa wakulima shambani.
Mkulima mmoja kutoka Stafford Matthew Weaver, amenukuliwa akisema
"Tulijua kuwa iwapo tunataka kupata ufanisi katika maandamano yetu ilikuwa lazima tufanye kitu cha kipekee ambacho pia kitawavutia watu na kuwapa sababu ya kuwachekesha.''
Weaver alisema wafugaji hao walitokea Derbyshire, Shropshire na Warwickshire .
Alisema kuwa bado wanapanga maandamano mengine katika maduka zaidi.
Kampuni ya maziwa ya Muller ilitangaza kuwa itapunguza bei ya maziwa kwa sababu soko lake limeporomoka
Toure ang'ara katika ushindi wa Man City, huyu jamaa anatimiza ndoto kiukweli
Yaya Toure aliiongoza Man City katika ushindi mnono dhidi ya West Brom ambapo Raheem Sterling aliyesajiliwa majira ya joto kwa dau la pauni milioni 49 akicheza mchezo wake wa kwanza kwa timu yake mpya.
Mkwaju wa Toure uliombabatiza mchezaji mwenzake David Silva ulikwenda pia kwenye miguu ya mlinzi wa West Brom Craig Dawson kabla ya kutinga nyavuni.
City waliendeleza kupanua ushindi wao baada ya Toure kupiga mkwaju mwingine uliokwenda kona ya juu na kuwa goli la pili.Nahodha Vincent Kompany alihitimisha ushindi huo kwa mpira wa kona na kuwa mwanzo mzuri katika dhamira ya kulipata taji la ligi kuu.
West Brom walikua na nafasi chache baada ya mpira wa kona uliopigwa na Chris Brunt kuunganishwa kwa kichwa na James Morrison ambayo ilidakwa vyema na Joe Hart.
City watakua wenyeji wa mabingwa wa amsimu uliopita Chelsea na inawezekana wakamkosa kiungo Yaya Toure aliyetolewa baada ya kupata maumivu ya misuli ya paja.
Wapiganaji wa Kikurdi washambuliwa na uturuki
Uturuki imeanzisha tena msururu wa mashambulizi dhidi ya wapiganaji wa Kikurdi yanayolenga maeneo 17 kusini mashariki, kwa mujibu wa jeshi
Maeneo hayo yapo mkoani Hakkari katika mpaka na Iran pamoja na Iraq.
Uturuki imushuhudia ghasia zaidi katika wiki za hivi karibuni kati ya wanajeshi na wapiganaji wa Kikurdi wanaotaka kujiondoa.
Mashambulio hayo yanajiri siku moja baada ya watu tisa kuuawa katika msururu wa mashambulizi dhidi ya vikosi vya usalama, wengine wakiwa katika eneo la kusini mashariki.
Mashambulizi ya jumatatu yanalaumiwa kutekelezwa na kundi la wakurdi la PKK.
Subscribe to:
Posts (Atom)
CAF kumuunga mkono INFANTINO Urais wa FIFA
Shirikisho la soka barani Afrika CAF linamuunga mkono Infantino Rais wa shirikisho la soka barani Africa (CAF) AHMAD AHMAD amesema shir...

-
Tuzo za VMA 2014 zimefanyika na mastaa wengi walifika kwenye hilo tukio. Listi ya mastaa hao iliongozwa na familia ya Jay Z na Beyon...
-
Luca Modric mchezaji bora wa mwaka wa FIFA Wameamua kumpa,ni baada ya kumdhurumu tuzo yake ya msimu wa 2009/10,mwaka huu wameona ai...
-
Mlinda mlango wa Derby Country akipangua mkwaju wa Phil Jones Timu ya DERBY COUNTY inayonolewa na nyota wa zamani wa CHELSEA, FRANK LAM...