Wednesday, 22 June 2016

Watu 30 wafariki dunia huko Libya hivi punde






Mapigano kati ya jeshi la Libya na wapiganaji wa Islamic State yamesababisha vifo vya zaidi ya watu 30.
Msemaji wa hospitali moja alisema kuwa wapiganaji 36 wameuawa huku wengine karibu 140 wakijeruhiwa katika mji wa Sirte ambao ni ngome ya Islamic state.
Wakati huo huo taarifa zinasema kuwa idadi ya watu waliouawa wakati mlipuko ulitokea katika ghala la silaha kwenye mji ulio magharibi wa Garabulli imeongezeka hadi watu 29.
Ghala hilo liliripotiwa kuwa ndani ya kambi inayotumiwa na wapiganaji kwenye mji wa Misrata pwani ya nchi.

Hatari: Korea Kaskazini yalipua makombora mengine.


Image copyrightAP
Image captionRais wa Korea Kaskazini Kim Jong Un
Korea Kusini inasema kuwa majirani zao Korea Kaskazini kwa mara nyingine tena, wameifanyia majaribio makombora yake mawili, hatua ya wazi ya kuonesha kukiuka hatua Umoja wa mataifa kuiwekea taifa hilo vikwazo vya kiuchumi. Taarifa zasema kombora la kwanza halikufanikiwa huku la pili likisafiri umbali wa kilomita mia nne.
Msemaji wa Waziri wa Umoja wa taifa wa Korea Kusini Joeng Joon-hee amesema majaribio hayo ni kukiuka vikwazo.
"Ulipuaji huo makombora kwa kutumia Teknolojia ya angani unakiuka maazimio ya Umoja wa mataifa. NIa ni uchokozi dhidi yetu. Tunashauri ni vyema kwa Korea Kaskazini kuzidisha nguvu katika kuimarisha amani katika eneo la rasi ya Korea na kwa maisha ya watu wake ambayo Korea kaskazini imekuwa ikisititiza kila wakati." Amesema
Naye waziri mkuu wa Japan Shinzo Abe amelaani hatua hiyo Korea ya Kaskazini.
"Leo kumelipuliwa makombora kwa kutumia teknolojia ya angani iliyotumika zamani huu ni ukiukwaji wa wazi wa azimio la Baraza la Usalama la Umoja wa mataifa. hatutarusu na tutaandaa azimio la kupinga hatua hiyo," amesema Waziri Mkuu huyo

CAF kumuunga mkono INFANTINO Urais wa FIFA

Shirikisho la soka barani Afrika CAF linamuunga mkono Infantino Rais wa shirikisho la soka barani Africa (CAF) AHMAD AHMAD amesema shir...