Friday, 21 September 2018

BUSWITA, MWINYI NA MAKAPU WARUDISHWA KUNDINI YANGA

Wachezaji wa Yanga katika moja ya mazoezi yao 

Taarifa mbalimbali zinasema kuwa uongozi wa klabu ya Yanga ya jiji DSM umewasamehe wachezaji wake watatu viungo Said Makapu na Pius Buswita pamoja na beki wa kushoto Haji Mwinyi ambao hawakuwa sehemu ya mchezo uliopita dhidi ya Stand United kwa kile kilichoelezwa kuwa ni utovu wa nidhamu.

Wachezaji hao waliondolewa kambini na Kocha Mkuu wa Yanga, Mkongomani Mwinyi Zahera kwa utovu wa nidhamu na sasa watakuwa sehemu ya kikosi kuelekea mechi zijazo za Ligi Kuu Bara ikiwemo ya mwishoni mwa juma dhidi ya Singida United.

Kocha wa Yanga Mwinyi Zahera

Imeelezwa kuwa wachezaji hao wameomba radhi kwa Kocha wao ambaye ameonekana kuwa mbogo kwa wale wote wanaoleta ujuaji ndani ya timu bila sababu za msingi.



No comments:

Post a Comment

CAF kumuunga mkono INFANTINO Urais wa FIFA

Shirikisho la soka barani Afrika CAF linamuunga mkono Infantino Rais wa shirikisho la soka barani Africa (CAF) AHMAD AHMAD amesema shir...