Monday, 24 September 2018

Tetesi za Soka Ulaya Jumatatu 24.09.2018: Smalling, Gotze, Zidane, Neves, Hazard

Chris Smalling
Mlinzi wa kati Manchester United Chris Smalling anataka kusaini mkataba mpya huko Old Trafford. Mchezaji huyo wa kimataifa wa ENGLAND mwenye miaka 28 amebakiza chini ya miezi 12 kwenye mkataba wake wa sasa. (Star)
Kiungo wa kati wa Borussia Dortmund Mjerumani Mario Gotze, 26, ameshuriwa kujiunga na meneja wake wa zamaniaJurgen Klopp huko Liverpool. (Sky Sports)
Mrio Gotze Kiungo mshambuliaji wa Borussia Dortmund 
David Beckham anafanya mazungumzo na mchezaji mwenzake wa zamani wakiwa Real Madrid Zinedine Zidane kuhusu kukisimamia klabu yake ya Inter Miami katika ligi ya MLS. (Mirror)

Beckham na Zidane enzi wakicheza pamoja Real Madrid
Kiungo wa kati wa Chelsea na Ubelgiji Eden Hazard, 27, anasema anahisi kuwa katika hali nzuri asilimia 200 licha ya kupumzishwa na meneja Maurizio Sarri kati kati ya wiki. Alirudi uwanjani akiwa kikosi cha kwanza wakati wa mechi iliyomalizika kwa sare siku ya Jumapili na West Ham. (Sky Sports)

Eden Hazard amekuwa kwenye kiwango murua sana msimu huu
Kipa mwenye miaka 25 wa Besiktas Loris Karius -ambaye yuko kwa mkopo huko Liverpool anasema anapata motisha kutoka kwa kipa wa zamani wa Ujerumani Olivier Kahn. (Bild - in German)
#BBC

No comments:

Post a Comment

CAF kumuunga mkono INFANTINO Urais wa FIFA

Shirikisho la soka barani Afrika CAF linamuunga mkono Infantino Rais wa shirikisho la soka barani Africa (CAF) AHMAD AHMAD amesema shir...