![]() |
Kocha wa Mtibwa Sugar Zuber Katwila |
Kocha wa MTIBWA SUGAR, ZUBER KATWILA amesema kama ilivyokuwa msimu uliopita kikosi chake kina malengo ya kunyakua taji mojawapo msimu huu miongoni mwa mashindano wanayoshiriki.
Akizungumza baada ya kumalizika kwa mchezo kati ya MTIBWA na AFRICAN LYON, KATWILA anasema wana kikosi kipana walichokiandaa vyema kwaajili kuwania mataji hivyo anaamini msimu huu hawatatoka patupu.
Katika mchezo wa jana uliochezwa kwenye dimba la uhuru jijin DSM MTIBWA waliwanyuka wenyeji AFRICAN LYON mabao MAWILI kwa BILA mabao yote yakifungwa na RAJAB ZAHIR na msimu uliopita walifanikiwa kunyakua ubingwa wa michuano ya kombe la shirikisho la soka nchini.
No comments:
Post a Comment