Monday, 24 September 2018

Mtibwa Sugar wapania mataji zaidi

Kocha wa Mtibwa Sugar Zuber Katwila
Kocha wa MTIBWA SUGAR, ZUBER KATWILA amesema kama ilivyokuwa msimu uliopita kikosi chake kina malengo ya kunyakua taji mojawapo msimu huu miongoni mwa mashindano wanayoshiriki.

Akizungumza baada ya kumalizika kwa mchezo kati ya MTIBWA na AFRICAN LYON, KATWILA anasema wana kikosi kipana walichokiandaa vyema kwaajili kuwania mataji hivyo anaamini msimu huu hawatatoka patupu. 

Katika mchezo wa jana uliochezwa kwenye dimba la uhuru jijin DSM MTIBWA waliwanyuka wenyeji AFRICAN LYON mabao MAWILI kwa BILA mabao yote yakifungwa na RAJAB ZAHIR na msimu uliopita walifanikiwa kunyakua ubingwa wa michuano ya kombe la shirikisho la soka nchini.

No comments:

Post a Comment

CAF kumuunga mkono INFANTINO Urais wa FIFA

Shirikisho la soka barani Afrika CAF linamuunga mkono Infantino Rais wa shirikisho la soka barani Africa (CAF) AHMAD AHMAD amesema shir...