Wabishi wa jiji la MWANZA, MBAO FC wamekwea kileleni kwenye msimamo wa ligi baada ya kuibuka na ushindi wa bao MOJA kwa BILA dhidi ya maafande wa jeshi la magereza nchini TANZANIA PRISONS.
Katika mchezo huo ulichezwa kwenye dimba la CCM KIRUMBA timu zote mbili zilitandaza kabumbu safi lakini bahati ilikuwa kwa MBAO ambao walipata bao la ushindi katika daika za lala salama likipachikwa kimiani na NDAKI ROBERT.
Matoke hayo yanawafanya MBAO kufikisha alama 13 baada ya kushuka dimbani mara SITA ambapo wameshinda michezo MINNE na kupoteza mchezo MMOJA huku wakitoka sare katika mchezo MMOJA.
Huko NANGWANDA SIJAONA mjini MTWARA wenye NDANDA FC wamekiona cha moto baada ya kutandikwa mabao MATATU kwa MOJA na chama la wana STAND UNITED matokeo yanayowafanya NDANDA kusalia katika nafasi ya 12 na alama zao SABA huku STAND wakipanda hadi katika nafasi ya NANE wakiwa na alama TISA.
Msimao wa Ligi Kuu baada ya michezo 3 ya jana
# | Standings | P | Pts |
---|---|---|---|
1 | 6 | 13 | |
2 | 4 | 12 | |
3 | 5 | 11 | |
4 | 5 | 10 | |
5 | 6 | 10 | |
6 | 6 | 9 | |
7 | 6 | 9 | |
8 | 6 | 9 | |
9 | 6 | 8 | |
10 | 5 | 7 | |
11 | 6 | 7 | |
12 | 6 | 7 | |
13 | 6 | 7 | |
14 | 5 | 6 | |
15 | 4 | 6 | |
16 | 6 | 6 | |
17 | 6 | 5 | |
18 | 5 | 2 | |
19 | 5 | 2 | |
20 | 6 | 1 |
No comments:
Post a Comment