![]() |
Mbwana Samatta akishangilia baada ya kufunga bao |
Nahodha wa timu ya taifa ya TANZANIA (Taifa Stars) MBWABA SAMATTA amefunga bao la pili katika ushindi wa mabao MAWILI kwa BILA waliopata timu ya GENK dhidi ya MALMO FC.
LEANDRO TROSSAD alianza kuifungia GENK bao la kwanza katika dakika ya 37 kabala ya SAMATTA kuihakikishia ushindi katika dakika ya 71 kwa kupachika bao la pili na kuzima matumaini ya MALMO ya kupata walau alama moja ya ugenini.
Katika baadhi ya matokeo mengine ya ligi ya YUROPA, SEVILLA wameitandika STANDARD LIEG mabao MATANO kwa moja, LUDOGORETS wamepokea kipigo cha mabao MATATU kwa MAWILI kutoka kwa BAYER 04 LEVERKUSEN, DINAMO ZAGREB wenyewe wameinyuka FENERBAHCE mabao MANNE kwa MOJA huku OLYIMPIC MARSEILE wakikiona cha moto nyumbani baada ya kutandikwa mabao MAWILI kwa MOJA na EINTRAINCHT FRANKFURT.
No comments:
Post a Comment