Wednesday, 3 June 2015

Blatter ajiuzulu , soma hii kuhusu soccer duniani


Sepp Blatter ameutingisha ulimwengu wa soka hapo jana kwa kusema kwamba anajiuzulu akiwa kama Rais wa Shirikisho la Sola la Kimataifa FIFA kutokana na uchunguzi wa rushwa ambao hivi sasa unamjumuisha hata kiongozi huyo mwenyewe binafsi mwenye umri wa miaka 79. Mtu aliezungumza kwa sharti la kutotajwa jina ameliambia shirika la habari la Uingereza Reuters hapo jana kwamba Blatter ambaye ameliongoza shirika hilo linalosimamia soka duniani tokea mwaka 1998 anachunguzwa na waendesha mashtaka wa Marekani na shirika la upepelezi nchini humo FBI. Msemaji wa FBI amekataa kulizungumzia suala hilo.Blatter raia wa Uswisi ambaye alikuwa ni mtu mwenye ushawishi mkubwa kwenye FIFA kwa miongo mingi ametangaza uamuzi wake wa kujiuzulu katika mkutano na waandishi wa habari ulioitishwa kwa haraka mjini Zurich hapo jana ikiwa ni siku sita baada ya polisi kuivamia hoteli moja mjini humo na kuwakamata maafisa kadhaa wa FIFA na ni siku nne baada ya kuchaguliwa tena kwa muhula wa tano akiwa rais wa FIFA. Amesema uchaguzi wa rais mpya wa FIFA utafanyika karibuni kadri inayowezekana lakini afisa mmoja wa FIFA amesema iwapo uchaguzi huo utafanyika mapema basi itakuwa mwezi wa Disemba.

No comments:

Post a Comment

CAF kumuunga mkono INFANTINO Urais wa FIFA

Shirikisho la soka barani Afrika CAF linamuunga mkono Infantino Rais wa shirikisho la soka barani Africa (CAF) AHMAD AHMAD amesema shir...