Maafisa wa mjini Delhi huko India wamepiga marufuku chakula aina ya
tambi ziitwazo ''Maggi noodles'' baada ya kufanyiwa uchunguzi na
kugunduliwa kuwa na kiwango kikubwa cha madini hatari aina ya lead.
Tambi
hizo za ''Maggi noodles'', ambazo zinatengenezwa na kampuni maarufu ya
Nestle ya huko India zilikuwa zikipendwa sana na kununuliwa kwa wingi na
walaji wengi .Kampuni yenyewe imejitetea kuwa vyakula vyao ni salama.
Lakini kufuatia tukio hilo la kupigwa marufuku kwa ''Maggi noodles'' hisa zao zimeporomoka katika soko lao la huko India .
No comments:
Post a Comment