Mchezaji chipukizi wa Kriketi raia wa Uingereza amefariki baada ya kuripotiwa kupigwa risasi na majambazi nchini Trinidad.
Adrian
St John , mwenye umri wa miaka 22 ambaye alikichezea chuo cha mafunzo
cha Chris Gayle mjini London anaaminika kufariki siku ya Jumapili.Mchezaji wa kriketi wa West Indies Gayle alichapisha ujumbe kwenye mtandao wa Twitter akisema " Ni habari mbaya kusikia ,Rambirambi zangu kwa familia na marafiki." Adrian St. John alikuwa nahodha katika chuo hicho.
Vyombo vya habari nchini humo vimeripoti kwamba Bwana St.John, alivamiwa baada ya kusimamisha gari lake ili kuwachukuwa rafiki zake alipovamiwa na kupigwa risasi.
No comments:
Post a Comment