Friday, 17 April 2015

arsene wenger amesema ushindi unahitajika mapema sana ,soma hapa



Arsene Wenger

Kocha wa Arsenal, Arsene Wenger ameitaka timu yake kutafuta ushindi wa mapema katika pambano la mwishoni mwa wiki hii Jumamosi dhidi ya Reading. Kocha huyo raia wa Ufaransa amesema kuwa vijana wake wanapaswa kuanza kwa kasi na nguvu katika mchezo huo utakaopigwa katika dimba la Wembley kama kweli wanahitaji kutetea taji lao.
Wenger amesema kwamba timu yake imejifunza msimu uliopita ambapo walihitaji penati kuishinda Wigan katika hatua ya nusu fainali kabla ya kutanguliwa goli mbili na wapinzani wao Hull City katika pambano la fainali ambapo hadi mwisho wa kipute hicho, waliibuka kidedea kwa ushindi wa mabao 3-2.
Mechi hiyo itakuwa ni nusu fainali ya kumi kwa mzee Wenger ,huku akidai kwamba Arsenal inajiamini hasa kutokana na kushinda mechi nane mfululizo. Nusu fainali ya pili itapigwa Jumapili ambapo Aston Villa itawakaribisha Liverpool.

No comments:

Post a Comment

CAF kumuunga mkono INFANTINO Urais wa FIFA

Shirikisho la soka barani Afrika CAF linamuunga mkono Infantino Rais wa shirikisho la soka barani Africa (CAF) AHMAD AHMAD amesema shir...