Thursday, 30 April 2015

Korea Kaskazini yaua maafisa kadhaa wa nyadhofa za juu



Rasi wa korea Kaskazini Kim Jong Un
Shirika la kiinteligensia la Korea kusini linasema utawala wa Korea kaskazini ,mwaka huu, umewauwa watu waliokuwa na nyadhfa za juu wapatao 15 , wanaodhaniwa kuwa wapinzani wa utawala wa kiongozi wa nchi hiyo Kim Jong-un, kama njia ya kunyamazisha upinzani nchi humo.
Mmoja wa wanaripotiwa kuuawa alikuwa naibu waziri aliyelalamikia na kukosoa sera ya misitu nchini humo.
Habari hizi zilitokea wakati shirika hilo la kiintelijensia lilipozungumza na kundi la watunga sheria wa huko Korea Kusini.
Korea kazkazini haijatoa kauli yoyote kuhusiana na madai hayo lakini uongozi wa nchi hiyo umewahi kuwauwa baadhi ya wapinzani wao.

No comments:

Post a Comment

CAF kumuunga mkono INFANTINO Urais wa FIFA

Shirikisho la soka barani Afrika CAF linamuunga mkono Infantino Rais wa shirikisho la soka barani Africa (CAF) AHMAD AHMAD amesema shir...