Uongozi wa ligi kuu ya England umeona ni vyema ukaonyesha kuridhishwa na kazi zake na kuamua kumpa tuzo kutokana na mchango wake mkubwa wa kuhamasisha soka la vijana Afrika kupitia michango yake na uamuzi wake wa kufungua Didier Drogba Foundation ambayo itakuwa ikifanya kazi ya kuwasaidia wenye matatizo.
Staa huyo wa soka wa Chelsea amepewa heshima hiyo kubwa na uongozi huo kama sehemu ya kumpongeza kwa kazi nzuri za kijamii anazofanya.
Tayari Drogba amejenga hospitali kubwa ya kisasa nchini kwao Ivory Coast.
No comments:
Post a Comment