Monday, 13 July 2015

baada ya usajili wa Schweinsteiger sasa ni zamu ya Schnederlin, tayari makubaliano yake.

Man United na Southampton wamekuwa na mazungumzo kwa muda wa wiki kadhaa sasa na hatimaye vilabu hivyo usiku wa kuamkia leo vilikubaliana bei ya uhamisho ya £25m kwa ajili ya Schnederlin.
Southampton walithibitisha kuikataa ofa ya kwanza ya Man United mapema wiki iliyopita, lakini yakiwa yamebaki masaa kadhaa kabla ya United kwenda kwenye Tour, hatimaye klabu hiyo imekubali ofa ya United.
   Schneiderlin aliyejiunga na Southampton mwaka 2008 akitokea Strasbourg kwa ada ya uhamisho wa £1.2m – jana usiku alifanyiwa vipimo vya afya na United na leo hii kabla ya safari wanategemea kutambulishwa rasmi yeye na mwenzie Bastian Schweinsteiger.

No comments:

Post a Comment

CAF kumuunga mkono INFANTINO Urais wa FIFA

Shirikisho la soka barani Afrika CAF linamuunga mkono Infantino Rais wa shirikisho la soka barani Africa (CAF) AHMAD AHMAD amesema shir...