Sunday, 17 January 2016

star tv , radio free africa na kiss fm zafungiwa kuruka hewani na TCRA ,soma sababu hapa.

Image captionTCRA
Mamlaka ya mawasiliano nchini Tanzania, TCRA imevifungia vituo vya Radio na Television kwa muda wa miezi 3 kikiwemo kituo cha Star TV, Radio free Afrika, Kiss Fm na Uhuru FM.
Vituo hivyo vimefungiwa kutoa huduma kwa miezi mitatu kila moja baada ya kushindwa kulipa kodi
Kulingana na mtandao wa jamii Forum,mnamo mwezi July 2015 Serikali ilitoa taarifa kwa umma na TCRA kwamba baadhi ya radio na Televisheni zipatazo 40 zinadaiwa ada na tozo mbalimbali.
Aidha Serikali iliviagiza vituo hivyo kuhakikisha kuwa vimelipa ada kufikia tarehe 31 mwezi Disemba 2015.
Hatahivyo baadhi ya vituo hivyo vililipa kodi hiyo mwanzoni mwa mwezi huu na wengine wakishindwa kulipa.
Kwa mujibu wa sheria unaposhindwa kulipa kodi TCRA huchukulia kwamba haupo.
TCRA sasa inasema kuwa iwapo miezi mitatu ijayo itakamilika bila malipo hayo kufanywa basi italazimika kuchukua hatua zaidi kama vile kuwapokonya leseni wahusika.
Ni vituo 11pekee kati ya vituo vilivyokuwa vikidaiwa na mamlaka hiyo vilivyotiii agizo hilo na kulipa.
Baadhi ya vituo hivyo ambavyo havitakuwa hewani kufikia jumatatu ni
1. Sibuka FM 2. Breez FM 3. Country FM 4. Ebony FM 5. Hot FM 6. Impact FM 7. Iringa Municipal TV 8. Kiss FM 9. Kitulo FM 10. Kifimbo FM 11. Mbeya City Municipal TV 12. Radio 5 13. Radio Free Afrika (RFA) 14. Musa Television Network 15. Pride FM radio 16. Radio Huruma 17. Radio Uhuru 18. Star TV 19. Rock FM Radio 20. Standard FM radio 21. Sumbawanga Municipal TV 22. Tanga City TV 23. Top Radio FM limited 24. Ulanga FM

mbwana Samatta apewa zawadi nono na serikali ya Tanzania, soma na itazame zawadi hiyo hapa




Samatta
Image captionSamatta aliibuka mfungaji mabao bora ligi ya klabu bingwa Afrika 2015

Mchezaji bora wa Afrika kwa wachezaji wa nyumbani Mbwana Samatta amekabidhiwa sehemu ya ardhi na serikali ya Tanzania kufuatia uhodari wake uliomwezesha kuondoka na tuzo hiyo na kuisaidia TP Mazembe kutwaa kombe la vilabu bingwa Afrika.
Mchezaji huyo pia alitunukiwa zawadi nyinginezo kwenye hafla iliyoandaliwa ili kusherekea mafanikio yake katika soka yaliyoiweka Tanzania katika ramani ya soka.
Hafla hiyo pia ilihudhuriwa na wadau wa michezo nchini Tazania wakiwemo waziri wa michezo Nape Nnauye na Thomas Ulimwengu ambaye ni mchezaji mwenza wa Samatta.
Amepewa kipande cha ardhi eneo la Kigamboni, Dar es Salaam na serikali kupitia wizara ya ardhi na nyumba.









Mchezaji huyo pia ameteuliwa nahodha mpya wa timu ya taifa Taifa Stars, nafasi ambayo awali ilishikiliwa na beki Nadir Haroub ‘Cannavaro’ anayeichezea klabu ya Yanga, kwa mujibu wa gazeti la Mwananchi.
Samatta, maarufu ‘Samagoal’ aliwapiku Robert Kadiaba na Bounedjah Baghdad wa Algeria anayeichezea klabu ya Etoile du Sahel na kutwaa tuzo hiyo.
Baada ya kupokea taji lake katika sherehe za kuwatuza wachezaji bora Afrika, mjini Abuja, Samatta alirejea Tanzania na baadaye kualikwa na Rais wa Zamani wa Tanzania Jakaya Kikwete.
Mnamo mwaka wa 2013, serikali ya Nigeria iliwakabidhi wachezaji wake sehemu ya ardhi mjini Abuja na pesa kwa kushinda kombe la Afcon.

Watu 21 wauawa nchini Burkina faso katika shambulizi la kushtukiza.ni siku chache baada ya kumpata raisi mpya.



Image copyrightAP
Image captionBurkina faso
Rais wa Burkina Faso amesema takriban watu 21 wameuwawa katika shambulio kwenye hoteli moja mjini Ogadugu na wanamgambo waliovamia hotel hiyo.
Roch Mark Christian Kabore amesema washambuliaji wanne waliovamia hotel hiyo waliuliwa ambapo wawili kati yao ni wanawake. Shambulio hilo lililotokea kwenye hotel ya Splendide kwenye mji mkuu wa Ouagadougou sasa limemalizwa.
Image copyrightAFP GETTY
Image captionbaadhi ya manusura
Waziri wa Ulinzi wa nchi hiyo amesema wanamgambo hao wameuwa watu kumi na nane kutoka mataifa mbalimbali. Zaidi ya watu mia moja na ishirini walikimbia hotel hiyo maarufu kwa watalii.
walionusurika wanasema wanamgambo hao walianza kupiga risasi kwenye jengo hilo na kisha kuliwasha moto.
Image copyrightReuters
Image captionWanajeshi maalum wa ufaransa
Kundi la Kigaidi la Al Qaeda kwenye ukingo eneo jangwa imesema lina husika na shambulio hilo.
Watu 126 waliokuwa mateka waliachiliwa huru katika hoteli ya Splendid iliopo katika mji mkuu wa taifa hilo la Magharibi mwa Afrika Ouagadougou, kwa mujibu wa waziri wa maswala ya ndani.
Image copyrightAP
Image captionEneo lililo karibu na jhoteli ya Splendid ilioshambuliwa
Wapiganaji wanne waliuawa aliongezea huku watu 21 wa mataifa 18 tofauti wakifariki wakati wa shambulio ambalo pia liliulenga mgahawa huo.
Vikosi maalum vya Ufaransa vinasaidia wanajeshi wa taifa hilo katika oparesheni hiyo.
Image captionEneo lililoshambuliwa
Rais wa Ufaransa Francois Hollande ameshtumu shambulio hilo la taifa hilo ambalo lilikuwa koloni yake hapo zamani.
Kundi la Al-Qaeda la islamic Maghreb{AQIM} limesema kuwa lilitekeleza shambulio hilo katika taifa hilo la Magharibi mwa Afrika.
Image captionHoteli ya Splendid
Mnamo mwezi Novemba shambulio la AQIM katika hoteli moja ya Bamako nchini Mali liliwauwa watu 19.

Wednesday, 13 January 2016

hivi punde zaidi ya watu 14 wauawa huko Pakistani kwa shambulio la bomu.tazama na soma hii


Polisi pakistanImage copyrightAFP
Image captionPolisi katika mji wa Quetta nchini Pakistani baada ya mlipuko wa bomu kwenye eneo la tukio
Takriban watu 14 wameuawa katika shambulio la bomu nje ya kituo cha kutoa chanjo ya ugonjwa wa kupooza(polio) katika mji wa kusini magharibi wa Quetta nchini Pakistani, kwa mujibu wa maafisa.
Wengi miongoni mwa waliouawa wanadhaniwa kuwa ni polisi waliokuwa wakilinda kliniki.
Mlipuko wa Bomu QuettaImage copyrightGetty
Image captionWanamgambo wa Islamic State wamekua wanasema chanjo za kupooza zinazuia uzazi nchini pakistani
Polisi wenye silaha huwalinda wahudumu wa afya wanaotoa chanjo ya kupooza nchini Pakistani ambao wamekua wakilengwa na mashambulio mabaya ya Islamic State miaka ya hivi karibuni.
Wanamgambo wa Islamic State wanapinga chanjo ya kupooza , wakisema ni mpango wa nchi za magharibi wa kufunga uzazi dhidi ya watoto wa Pakistani.
Pakistan quettaImage copyrightAP
Image captionPakistan na Afghanstan ndio nchi pekee zenye maambukizi mengi ya maradhi ya kupooza zaidi duniani
Pakistan na Afghanistan ni nchi pekee zilizosalia zenye visa vingi vya marathi ya kupooza.
Mlipuko wa bomu hilo ulitokea mapema subuhi wakati wahudumu wa kutoa chanjo na maafisa wa usalama walipokua wakiripoti kazini kabla ya kuelekea nje kwa mizunguko ya kutoa chanjo hiyo , amesema Sarfaraz Bugti, waziri katika jimbo la Balochistan ambalo Quetta ni mji mkuu wake.
Polisi katika eneo hilo wanasema kuwa mlipuko huo uliwauwa polisi 12, mwanajeshi mmoja na raia mmoja. Watu wapao 20 wamejeruhiwa.

Thursday, 7 January 2016

tazama ngoma mpya ya wiz khalifa hapa na dowload hapa iwe yako.

tazama hapa Obama alivyotokwa machozi akizungumzia silaha.

Rais Barack Obama alitokwa na machozi jana alipokuwa akitetea kufanyiwa mabadiliko kwa sheria za udhibiti wa silaha nchini Marekani.

ObamaImage copyrightAP
Image captionObama aliwaambia Wamarekani kwamba mageuzi anayotekeleza ni ya kuwafaa
ObamaImage copyrightReuters
Hii ni kutokana na ongezeko la watu kushambuliwa kwa risasi nchini humo.

ObamaImage copyrightReuters
Kiongozi huyo anayemaliza muhula wake wa pili mwaka huu alisema kwa sasa yeye hatafuti kura.
Obama anataka watu wote wanaouza silaha washurutishwe kuwa wakipekua na kuchunguza historia ya watu wanaowauzia silaha.
Kwa sasa, takwa hilo hugusa tu wauzaji silaha waliosajiliwa.

Image copyrightGetty
Wale hawajasajiliwa, hutakiwa kuwauliza tu wanunuzi watarajiwa iwapo wamewahi kupatikana na makosa ya uhalifu au kama wana matatizo ya kiakili.

Image copyrightAP
Hatua hiyo ya Rais Obama imepingwa vikali na baadhi ya viongozi wakuu wa chama cha Republican wanaosema inaingilia uhuru wa kikatiba wa Wamarekani.

Wednesday, 6 January 2016

baada ya Korea Kaskazini kulipua bomu la haidrojeni,UN kuichukulia hatua kali.soma hii ni muhumu sana




Image copyrightAPTN
Image captionTangazo kuhusiana na jaribio hilo la bomu la Hydrogen la Korea Kaskazini
Siku moja baada ya Korea Kaskazini kufanya jaribio la bomu la haidrojeni, Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limekubaliana kuanza mikakati ya kuiwekea vikwazo.
Hata hivyo baadhi ya Wataalamu wameonyesha kuwa na wasi wasi kuhusu jaribio la sasa la nyuklia la Korea Kaskazini ambalo ni la nne katika mwongo mmoja, wakisema huenda lisiwe la haidrojeni kutokana na mlipuko uliotokea.
Bomu la hydrojeni ni moja ya mabomu hatari ya jamii atomiki au nyuklia yenye nguvu zaidi. Wataalam wanasema bomu hili la hydrojeni lina uwezo mkubwa kiasi kwamba linaweza kulipua mji mmoja wote kwa mlipuko mmoja.
Kufuatia jaribio hilo jamii ya kimataifa imendelea kulaani tukio hilo Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ambaye pia ni Waziri wa zamani wa Mambo ya nje ya Korea Kusini Ban Ki moon akisema jaribio hilo la bomu la nyuklia ni hatua ya kuogopesha.
"Hili jaribio kwa mara nyingine limekiuka maazimio kadhaa ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa pamoja na wito wa pamoja wa jamii ya kimataifa kukomesha vitendo hivyo. Pia linakwenda kinyume kabisa na utamaduni wa kimataifa wa majaribio ya mabomu ya nyuklia. Tendo hilo linaonekana ni la kuogopesha kwa usalama wa kanda na kupuuza juhudi za kimataifa za kuacha kutengeneza silaha za nyuklia. Ninalaani kwa nguvu jambo hilo."


Image copyright
Huko Marekani nayo Ikulu ya White house imesema utafiti wake wa awali kuhusu jaribio hilo la bomu nyuklia la Korea ya Kaskazini hauthibitishi madai kwamba nchi hiyo imefanikiwa kulipua bomu la haidrojeni.
Msemaji wa White house Josh Earnest amesema Korea ya Kaskazini inafaa kutengwa zaidi kama itaendelea na matendo yake ya ukiukaji wa makubaliano ya kimataifa kuhusu silaha za nyuklia ikiwa ni pamoja na kufanya majaribio makombora ya angani.
"Tumesikitishwa sana na matokeo ya uharibifu wa amani na utulivu baada ya matendo ya ukiukaji wa Korea Kaskazini kuzidi kuongezeka. China na Urusi nao pia wamesikitishwa. Ndio maana tunafanya bidii kuiweka pamoja jamii ya kimataifa na kuweka wazi kwa Korea Kaskazini kwamba njia ni moja tu iliyobaki ambayo ni nzuri kwa raia wa Korea Kaskazini, ambayo itakuwa nzuri kwa uchumi wa Korea kaskazini, nzuri kwa nchi Korea Kaskazini kwa maana ya uwezo wao wa kujihusisha na jamii ya kimataifa."


tazama hapa Obama alivyotokwa machozi akizungumzia silaha.

Rais Barack Obama alitokwa na machozi jana alipokuwa akitetea kufanyiwa mabadiliko kwa sheria za udhibiti wa silaha nchini Marekani.

ObamaImage copyrightAP
Image captionObama aliwaambia Wamarekani kwamba mageuzi anayotekeleza ni ya kuwafaa
ObamaImage copyrightReuters
Hii ni kutokana na ongezeko la watu kushambuliwa kwa risasi nchini humo.

ObamaImage copyrightReuters
Kiongozi huyo anayemaliza muhula wake wa pili mwaka huu alisema kwa sasa yeye hatafuti kura.
Obama anataka watu wote wanaouza silaha washurutishwe kuwa wakipekua na kuchunguza historia ya watu wanaowauzia silaha.
Kwa sasa, takwa hilo hugusa tu wauzaji silaha waliosajiliwa.

Image copyrightGetty
Wale hawajasajiliwa, hutakiwa kuwauliza tu wanunuzi watarajiwa iwapo wamewahi kupatikana na makosa ya uhalifu au kama wana matatizo ya kiakili.

Image copyrightAP
Hatua hiyo ya Rais Obama imepingwa vikali na baadhi ya viongozi wakuu wa chama cha Republican wanaosema inaingilia uhuru wa kikatiba wa Wamarekani.

CAF kumuunga mkono INFANTINO Urais wa FIFA

Shirikisho la soka barani Afrika CAF linamuunga mkono Infantino Rais wa shirikisho la soka barani Africa (CAF) AHMAD AHMAD amesema shir...