Monday, 28 March 2016

hivi punde Milio ya risasi jengo la Bunge Marekani, tazama na soma hii


 

 Image copyright d Image caption Jengo la Bunge la Marekani Capitol Hill

Kuna taarifa za milio ya risasi katika viunga vya jengo la Makao Makuu ya Bunge la Congress, US Capitol Hill.
Mashuhuda wanasema wameambiwa kwa vipaza sauti kuwa kila mtu ajifiche.
Taarifa za hivi punde zinasema mtu huyo mwenye silaha amekamatwa na polisi mmoja amepigwa risasi na kujeruhiwa.
Waandishi wa Habari waliokuwa kwenye eneo jengo la Bunge wameambiwa waendelea kubaki ndani.
Ikulu ya White House nayo imefungwa. Msemaji wa Polisi katika Jengo la Bunge hajasema lolote lakini ameahidi polisi kutoa taarifa za tukio hilo wakati wowote.

No comments:

Post a Comment

CAF kumuunga mkono INFANTINO Urais wa FIFA

Shirikisho la soka barani Afrika CAF linamuunga mkono Infantino Rais wa shirikisho la soka barani Africa (CAF) AHMAD AHMAD amesema shir...