Polisi ya nchi hiyo imeripoti kuwa, watu wenye silaha wamemshambulia mkuu wa ofisi ya ardhi katika eneo la Melaky na kumuua pamoja na rafiki yake. Katika hujuma hiyo watu wengine kadhaa pia wamejeruhiwa. Polisi wamesema kuwa, washambuliaji hao walianza kufyatua risasi kuilenga gari iliyokuwa imembeba afisa huyo wa ardhi pamoja na watu wengine aliokuwa ameambatana nao. Habari zaidi zinasema kuwa, licha ya polisi kufika eneo la tukio mapema, lakini walishindwa kukabiliana na watu hao wenye silaha, huku wakitoweka bila ya kutiwa mbaroni. Polisi imetangaza kuwa inaendelea kuwasaka wahusika wa hujuma hiyo, ambayo hadi sasa bado sababu za utekelezwaji wake hazijulikani, ingawa masuala ya kisiasa yanatajwa kuwa moja ya sababu hizo.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
CAF kumuunga mkono INFANTINO Urais wa FIFA
Shirikisho la soka barani Afrika CAF linamuunga mkono Infantino Rais wa shirikisho la soka barani Africa (CAF) AHMAD AHMAD amesema shir...
-
Image caption Uganda haipaswi kuzuia upinzani, Obasanjo Aliyekuwa rais wa zamani wa Nigeria, Olusegun Obasanjo, ametaka pande zote pinza...
-
Tuzo za VMA 2014 zimefanyika na mastaa wengi walifika kwenye hilo tukio. Listi ya mastaa hao iliongozwa na familia ya Jay Z na Beyon...
No comments:
Post a Comment