Serikali ya
Uingereza imewaonya wapenzi wa jinsia moja wanaosafiri kuelekea Marekani
kutokana na sheria dhidi yao katika majimbo ya North Carolina and
Mississippi.
Marekani ni jamii kubwa ilio na maoni tofauti.Sheria
mpya zilizopitishwa katika majimbo hayo zinaruhusu wafanyibiashara
kuamua iwapo wanaweza kuwahudumia watu wa jinsia hiyo au la.Ushauri huo umetoka katika afisi ya maswala ya kigeni ya Uingereza.
Katika jimbo la Carolina,sheria iliopitishwa na Gavana Pat McCrory inasema kuwa watu waliobadili jinsia watumie msaala wa kuogea kulingana na jinsia yao iliopo katika vyeti vyao vya kuzaliwa.
Sheria ya Mississippi pia ina sheria kama hiyo na inawalinda wafanyibiashara wengi kytoshtakiwa kwa kukataa kuwauzia wapenzi wa jinsia moja.
No comments:
Post a Comment